Habari za Punde

Tushirikiane Kutokomeza Ukeketaji kwa Watoto wa Kike - Ummy Mwalimu.

Mhe. Waziri wa Afya.Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumzia uzefu wa Tanzania katika kukabiliana na tatizo la  ukeketaji akiwa na wazungumzaji wengine katika Meza Kuu, kutoka kushoto ni Mke wa  Rais wa Burkina Faso Bi. Sika Bella Kabore,  Bw. Benoit Kalasi (UNFPA), Bi.Emma Bonino Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje Italia.
Sehemu ya washiriki wa Mkutano na majadiliano  kuhusu utokomezaji wa vitendo vya ukeketaji na uhusiano wake na utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu. Mkutano huu  uliandaliwa kwa pamoja na Wakilishi za  Kudumu za Tanzania, Burkina Faso, Italy, Iran, UNFPA na UNCEF
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii, Mhe. Peter Serukamba akifuatilia majadiliano kuhusu tatizo la  ukeketaji  na  adhari zake wa afya na maendeleo ya mtoto wa kike na mwanamke.
Wajumbe kutoka Serikali ya Mapinduzi nao wakifuatilia majadiliano  yaliyovutia washiriki wengi kuhusu madhara  yatokanayo  na ukeketaji na namna gani  jamii inatakiwa kushirikiana kutokoza tatizo hilo. 
  Mhe Waziri Ummy  Mwalimu akibadilishana mawazo na washiriki wa majadiliano kuhusu ukeketaji.
Waziri  Mwalimu akibadilishana  mawazo na Waziri  mwenzie Sicily Kariuki kutoka  Kenya

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.