STATE HOUSE
ZANZIBAR
OFFICE OF THE
PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 10.4.2016
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaapisha Mawaziri na Manaibu
Mawaziri wa Wizara 13 za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na Mawaziri
wasiokuwa na Wizara Maalum ambao pia ni Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi.
Hafla hiyo ilifanyika katika viwanja vya
Ikulu mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa vyama na
Serikali pamoja na wananchi kadhaa ambapo miongoni mwa waliohudhuria ni Makamu
wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Othman
Makungu, Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Zubeir Ali Maulid.
Wengine ni Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar
Mhe. Said Hassan Said, Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji na Mkuu
wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe. Abdalla
Mwinyi Khamis. Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib pamoja
na viongozi wa vikosi vya Ulinzi.
Walioapishwa katika hafla hiyo ni Waziri,
Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Issa Haji Ussi Gavu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Haroun Ali Suleiman. Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Haji Omar Kheri, Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe. Mohammed Aboud Mohammed.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Khalid
Salum Mohammed, Waziri wa Afya Mhe. Mahmoud Thabit Kombo, Waziri wa Elimu na
Mafunzo ya Amali Mhe. Riziki Pembe Juma pamoja na Waziri wa Kazi, Uwezeshaji,
Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Mhe. Moudline Castico.
Wengine ni Waziri wa Biashara, Viwanda na
Masoko Mhe. Balozi Amina Salum Ali, Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na
Usafirishaji Mhe. Balozi Ali Abeid A. Karume. Waziri wa Kilimo, Maliasili,
Mifugo na Uvuvi Mhe. Hamad Rashid Mohammed. Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni
na Michezo Mhe. Rashid Ali Juma na Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira
Mhe. Salama Aboud Talib.
Kwa upande wa Manaibu Waziri ni Naibu
Waziri wa Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe.
Khamis Juma Maalim. Naibu Waziri wa Afya Mhe. Harusi Said Suleiman na Naibu
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Mhe. Mmanga Mjengo Mjawiri.
Wengine ni Naibu Waziri wa Ujenzi,
Mawasiliano na Usafirishaji Mhe. Mohammed Ahmed Salum. Naibu Waziri wa Kilimo,
Maliasili, Mifugo nan Uvuvi Mhe. Lulu Msham Abdulla, Naibu Waziri wa Habari,
Utalii, Utamaduni na Michezo Mhe. Bibi Choum Kombo Khamis na Naibu Waziri wa
Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira Mhe. Juma Makungu Juma.
Aidha, Dk. Shein amewaapisha
Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi na Mawaziri Wasiokuwa na Wizara Maalum akiwemo
Mhe. Said Soud Said kuwa Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Waziri Asiekuwa na
Wizara Maalum pamoja na Mhe. Juma Ali Khatib Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na
Waziri Asiekuwa na Wizara Maalum.
Kwa uwezo aliopewa chini ya Vifungu 42,
43,44 na 47 vya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Dk. Shein ameunda Wizara 13
za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kuwateua Mawaziri na Manaibu Mawaziri
wa Wizara hizo pamoja na Mawaziri Wasiokuwa na Wizara Maalum na Wajumbe wa
Baraza la Mapinduzi.
Rajab Mkasaba,
Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment