Habari za Punde

Zantel yatoa msaada wa vifaa mbalimbali kusaidia kambi za ugonjwa wa kipindupindu Zanzibar.

Mkuu wa Zantel Zanzibar, Mohamed Mussa Baucha akiongea kwenye hafla hiyo

 Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mahmoud Thabit Kombo (katikati) akizungumza kwenye hafla ya kupokea msaada wa vifaa kutoka Zantel
Kulia ni Mkuu wa Zantel Zanzibar, Mohamed Mussa Baucha na Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dk.Juma Malik.

  Mkuu wa Zantel Zanzibar, Mohamed Mussa Baucha (kulia) akimkabidhi vifaa mbalimbali Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mahmoud Thabit Kombo.
 Mohamed Mussa Baucha akikabidhi vifaa kwa Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mahmoud Thabit Kombo.
Waziri wa Afya wa Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akikabidhi moja ya vifaa hivyo vilivyotolewa na Zantel kwa Dk.Fadhil Mohamed, Daktari dhamana kanda ya Unguja ambaye pia ni msimamizi mkuu wa kambi za wagonjwa wa kipindupindu


Kampuni ya simu ya mikononi ya Zantel leo imetoa msaada wa vifaa vya usafi kwa ajili ya kusaidia juhudi za kupambana na kipindupindu za Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kwa ajili ya kambi za kipindupindu visiwani humo.

Vifaa hivyo ambavyo vimekabidhiwa kwa Wizara ya Afya vimegharimu jumla ya shlingi milioni 11, ni pamoja na matanki ya kuhifadhia maji, vitanda vya kamba, pampu ya kisima, mabomba ya kunyunyizia dawa, maturubali mazito, maboksi ya gloves na mafuta ya petroli lita 3,000 kwa ajili ya magari ya kuhudumia kambi za kipindupindu.


Akizungumza wakati wa kupokea vifaa hivyo, Waziri wa Afya, Mheshimiwa Mahmoud Thabit Kombo amesema ugonjwa wa kipindupindu ambao mpaka sasa umesabababisha vifo vya watu 53 utatoweka visiwani Zanzibar baada ya wiki tatu zijazo.

‘Kwa kiasi kikubwa juhudi zetu za kupambana na kipindupindu kwa kushirikiana na mamlaka mbalimbali zimeanza kufanikiwa, na tunaomba wadau wengine wazidi kujitokeza kutuunga mkono’ alisema Mahmoud.

Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya kampuni ya Zantel, Mkuu wa kampuni ya Zantel upande wa Zanzibar, Mohammed Mussa amesema kampuni yake inajivunia kushirikiana na serikali ya Zanzibar kupambana na ugonjwa wa kipindupindu ambapo ameeleza kuwa tarehe 23 na 24 mwezi uliopita kampuni ya Zantel imetuma ujumbe kwa wateja wake zaidi ya laki sita na nusu juu ya kujikinga na ugonjwa huo.

‘Tunawaomba wananchi waendelee kudumisha kanuni za usafi ikiwemo kuweka mazingira safi, kuchemsha maji ya kunywa, kunawa mikono kabla ya kula na baada ya kutoka kufanya haja ili kujikinga na janga la kipindupindu’ alisema Mussa.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.