Habari za Punde

Mkutano Mkubwa wa Kitaifa Kumuombea Rais na Taifa kwa Ujumla Kufanyika Agosti 25 Chato Mkoani Geita.


Mwenyekiti wa Good News for All Ministry, Askofu Dk.Charles Gadi (wa tatu kushoto), akiongoza maombi baada ya kuzungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu mkutano mkubwa wa maombi ya kitaifa wa kumuombea Rais Dk.John Magufuli na Serikali, utakaofanyika Agosti 25 Chato mkoani Geita. Kutoka kushoto ni Wachungaji Denis Kimbilo, Leons Kajuna, Palemo Massawe, Andrew Thomas na Denis Komba.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.



Na Dotto Mwaibale
VIONGOZI wa Good News for All Ministry  wameandaa mkutano mkubwa wa kitaifa wa maombi ya kumuombea Rais Dk. John Magufuli na Taifa kwa ujumba maombi yanayotarajiwa kufanyika Agosti 25 Chato mkoani Geita.


Katika hatua nyingine viongozi hao wamesema wanaunga mkono azma ya Rais Magufuli ya kuhamishia serikali Dodoma kwani ni jambo ambalo lilikuwa likisubiriwa kwa muda mrefu, hivyo wameandaa mpango wa kumuombea kwa siku 1001 sawa na miaka mitatu ili afanikiwe.


Wakizungumza Dar es Salaam leo asubuhi  viongozi hao kutoka Good News for All Ministry walisema uamuzi wakuanzisha mchakato wa kuhamisha serikalini jambo la kijasiri na unapaswa kuungwa mkono na watanzania wote kwani ni maono ya Baba wa taifa Julius Nyerere.


Askofu Dk. Charles Gadi alisema tangu Baba wataifa kutangaza azma hiyo serikali zilizotangulia zimefanya jitihada mbalimbali za kuimarisha mji wa Dodoma ili uweze kutumika kama mji mkuu na sasa umefika wakati muhafaka.


“Sisi kama viongozi wa dini tupo nyuma yake na tunaongeza nguvu zetu natunatoa wito kwa watu  wotewaserikali kuhamia Dodoma, kwani jambo hili litaharakisha maendeleo katika mikoa ya pembezoni,” alisema.


AidhaAskofu huyo  alishangazwa na uvumi kuwa endepo baadhi ya watendaji waserikali wakihamia Dodoma kutakwepo na migogoro katika ndoa nyingi kutokana na kutengana kwa baadhi ya familia.


Alisema ni vyema watu wakaheshimu maadili na kuishika misingi, kwani kusafiri hakukufanyi ‘ukachepuka’.


“Hata ukiwa hapa Dar es Salaam unaweza kuchepuka tu,silazimaiwe Dodoma, mambo yaliyowazi ni yetu ila ya liyofichwa ni ya Mungu,” alisema.


Mchungaji Leons Kajuna alisema RaisMagufuli hastishike na kelele za watu zinazobeza azma  yake kwani kawaida ya watu kupinga jambo linaloanzishwa kabla hawajaona mafanikio yake.
“Si wakati tena wakukaa na kunung’unika kuna vitu serikali ikishaamua ni kuvipokea kwa shukurani, 
kwani kufanya hivyo niishara ya nidhamu,” alisema.


Askofu Dk. Charles Gadi alisema mpango waliyo  uanzisha wakumuombea  Rais kwa siku 1001 utaanzia katika mkoa wa Geita  wilayaniChato na   unatarajiwa kuhudhuriwa na mkuu wa mkoa huo.



“Tutamuombea Rais katika uongozi wake kuwepo na mvua

za kutosha kwani uwepo wa mvua niishara uongozi umekubalika, nauwepowamvuautaondoanjaanamgawowaumeme,” alisema.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.