Timu ya wazungumzaji wa Fursa
wakiwa katika picha ya pamoja na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja
wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa
Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez pamoja
na Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa, Hoyce Temu.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja
wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa
Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez
akizungumza na vijana waliohudhuria semina ya Fursa mkoani Dodoma mwishoni
mwa wiki hii
Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja
wa Mataifa
(UN) nchini, Hoyce Temu akitoa mafunzo ya
malengo ya maendeleo enedelevu kwa vijana wa Dodoma waliojitokeza wakati
wa semina za Fursa zilizofanyika Dodoma mwishoni mwa wiki hii
Baadhi ya vijana waliojitokeza kwa
wingi kuhudhuria mafunzo ya Fursa mwishoni mwa wiki hii mkoani Dodoma
Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na
Ajira, Mhe. Antony Mavunde akizungumza na vijana
wakati akifungua semina ya Fursa iliyofanyika Dodoma mwishoni mwa wiki
Mmoja wa wazungumzaji wa semina
za Fursa, Yahaya Nawanda akizungumza na vijana kwenye siku ya pili ya
mafunzo ya kilimo na ufugaji yaliyofanyika mwishoni mwa wiki hii mkoani
Dodoma.
Mwanzilishi wa Fursa , Ruge Mutahaba akizungumza na vijana wakati wa siku ya pili ya semina za Fursa zilizofanyika Dodoma mwishoni mwa wiki hii

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi mmoja wa vijana waliopata mafunzo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa mjini Dodoma. Anayetazama kushoto ni Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu.

Baadhi ya vijana waliopata mafunzo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa mjini Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez pamoja na Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu.
No comments:
Post a Comment