Habari za Punde

Wahitimu mafunzo ya ualimu kupitia elimu masafa watakiwa kujiendeleza zaidi

Maalim Mkubwa Ahmed Omar akizungumza na wahitimu wa Mafunzo ya Ualimu katika Mahafali ya nne ya Mafunzo ya Ualimu kupitia Elimu Masafa yaliyofanyika katika ukumbi wa TC Michakaeni. Awali Mratibu wa Mratibu wa Kituo cha Walimu Michakaeni Ndugu Rashidi Juma Khamis

Na Ali Othman
Mratibu wa idara ya mafunzo ya ualimu Pemba Malim Mkubwa Ahmed Omar Amewasihi wahitimu wa  mafunzo ya ualimu kupitia elimu masafa kuhakikisha kwamba wanaitumia fursa ya elimu waliyoipata katika vituo vya walimu (TC) kujiendeleza zaidi katika ngazi nyengine za kitaaluma.
Akizungumza katika mahafali ya nne ya Mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti kupitia elimu masafa yaliyofanyika katika ukumbi wa TC Michakaeni Chake Chake Pemba, Malim Mkubwa amewapongeza wahitimu hao kwa juhudi na uvumilivu wao uliowapelekea kumaliza mafunzo kwa ufanisi.
“Kazi hii nikazi kubwa sana, mawimbi yake nimazito, nawapongeza kwa kuweza kuvuka salama na kwa mafanikio” Amesema Malim Mkubwa.
Mratibu huyo wa idara ya mafunzo ya ualimu Pemba amewataka wahitimu hao kuonesha mabadiliko katika utendaji wa kazi zao akiwathibitishia kwamba kwasasa wameiva.
Aidha Malim Mkubwa amempongeza  Mratibu wa Kituo cha Walimu Michakaeni Ndugu Rashidi Juma Khamis kwa kusimamia ipasavyo majukumu yake. Akitoa mfano wa majukumu hayo Malim Mkubwa amesema Mratibu huyo amekua wakwanza kuwasilisha marejesho kila mara yanapohitajika.
Awali Mratibu wa Kituo cha Walimu Michakaeni Ndugu Rashidi Juma Khamis ametoa takwimu ya wahitimu ambapo jumla yao ni 64 ikiwa 16 kati yao walisomea lugha, 27 Walisomea sayansi ya jamii na 21 kati yao walisomea sayansi.
Nae Kaimu Mratibu wa Elimu Masafa Pemba Malim Hemed Said  Masoud ameelezea kuridhishwa kwake kutokana na mwenendo mzima wa mafunzo ya ualimu kupitia elimu masafa na kuahidi kusimamia ipasavyo wanafunzi waliodahiliwa kuendelea na mafunzo hayo kwa awamu nyengine.
Hii ni mahafali ya nne ya Wahitimu wa elimu masafa kupitia vituo vya walimu TC, ambapo jumla ya wanafunzi 64 wamehitimu mafunzo hayo.

Malim Mkubwa Ahmed Omar akizungumza na wahitimu wa Mafunzo ya Ualimu katika Mahafali ya nne ya Mafunzo ya Ualimu kupitia Elimu Masafa yaliyofanyika katika ukumbi wa TC Michakaeni Awali Mratibu wa Mratibu wa Kituo cha Walimu Michakaeni Ndugu Rashidi Juma Khamis

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.