Habari za Punde

Mwanamke adakwa na kete 3621 zinazodhaniwa ni za dawa za kulevya Mkoani


NA HAJI NASSOR, PEMBA
JESHI la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba, linamshikilia kijana Zuhura Ahmed Ali (29) mkaazi wa Jadida wilaya ya Wete, akidaiwa kukutwa na kete 3, 621 zinazodhaniwa kuwa ni dawa za kulevya.
Mwanamke huyo alikamatwa kiulani kwenye kuzuizi cha barabara eneo la Mbuaguani Mkoani, wakati alipoteremka kwenye gari ya abiria, iliokuwa imesheni abiria ili akapandie mbele, ndipo alipoitwa na Polisi aliekuwepo hapo, kwa lengo la kumsalimiana ingawa alionekana na wasiwasi.
Iliofahamika kuwa, wakati Polisi huyo na mwanamke wakiendelea kusalimiana kikawaida, alionekana na hofu kubwa na kutetemeka ndipo alipoitwa na kutii amri, ingawa alitaka kujisaidia na na kutoa kauli za ubabaifu kama mtu alie usingizini.
Baada ya kudai kutaka kujisaidia mara haja kubwa mara haja ndogo, ndipo Plisi aliekuwepo zamu, alimtilia mashaka na kumkabidhi kwa mkusanya mapato mwanamke mwenzake aliekuwepo kwenye kizuizi hicho, na wote kwenda kituo cha Polisi Mkoani na kufanyiwa upekuzi.
Mara baada ya kufika ndani ya Kituo hicho na kufanyiwa upekuzi na Polisi wanawake, kijana huyo aliekuwa amevalia shungi kubwa jeusi alikutikana na hizo kete 3,621 zinazoaminika kuwa ni dawa za kulevya.
Kamanda wa Polisi Mkoa huo Sheihan Mohamed Sheihan, alikiri kukamatwa kwa mwanamke huyo, na kusema mfuko uliokuwa na dawa hizo, zinazodhaniwa kuwa ni za kulevya, aliufunga vyema kwenye tumbo lake.
Alisema aliziweka vyema kiasi ambacho hata akienda mbio haziwezi kutoka na kisha kuzitia ndani ya mkoba na kuzibana vyema kwa shungi lake kubwa jeusi, alilokuwa amelivaa kwa njia ya kama ya kujistiri.
“Hata askari waliomkamata walipata wasisi kwamba huwenda hizo kete ni zake, maana hazionyeshi kuwa ni mzigo kapewa na mtu anaemfahamu ampelekee Jadida Wete, maana ulifungwa vyema”,alisema Kamanda.
Aidha  Kamanda huyo wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba, aliwaambia waandishi wa habari kuwa, tukio hilo lililtokea majira ya saa 5:00 asubuhi kwenye kizuizi cha barabara ya Mkoani Mbuguani.
Alisema tayari mwananmke huyo ameshahojiwa na wanalojina na mtu aliemtaja kumpa mfuko huo, ambapo wote baada ya taratibu kukamilika watafikishwa mahakamani.
Kwa upande wake mwanamke huyo Zuhura Ahmed Ali (29) mkaazi wa Jadida Wete, alisema mfuko huo sio wa kweke na amepewa na mtu njiani amkamatie bila ya kujua ni mzigo wa aina gani.
Alisema yeye baada ya kupewa hakujua nini kilichokuwemo ndani yake, na baada ya kukamatwa nao alishangaa kuambiwa kuwa mna dawa za kulevya.

Wakati mtuhumiwa huyo akieleza hayo, Jeshi la Polisi limesema lilishangaa kuona kuwa mfuko huo mwanamke huyo sio wake, ingawa aliuhifadhi kwenye tumbo kwa nje na kuufunga na kisha kuuvalia shungi.

Baadhi ya wananchi wa Mkoa wa kusini Pemba, wamesema lazima Jeshi la Polisi liongeze juhudi za kuyasaka madawa ya kulevya, kutokana na kushamiria katika siku za hivi karibuni

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.