Mkuu wa kitengo cha Tehama kutoka Radio Times Fm
Bw. Dickson George Zuri (wapili kulia) akimuonyesha Waziri wa Habari Utamaduni
Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) moja ya mtambo unaotumika
kurushia matangazo katika studio za Times Fm alipofanya ziara katika radio hiyo
leo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari
Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akizungumza na
watumishi wa Radio Times Fm (hawapo pichani) alipofanya ziara katika radio hiyo
leo Jijini Dar es Salaam. Kushuto ni Mkurugenzi wa vipindi kutoka Times Fm Bw.
Amani Missana
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.
Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na wananchi moja kwa moja kupitia Studio za
Times Fm alipofanya ziara katika radio hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari
Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akimsikiliza Mchambuzi
Mkaazi kutoka Radio Times Fm Dkt. Bravious Kahyoza (kushoto) alipofanya ziara
katika radio hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Wapili kulia ni Mkurugenzi wa
vipindi kutoka Times Fm Bw. Amani Missana
Waziri wa Habari
Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (wapili kushoto) katika
picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Radio Times Fm baada ya kufanya ziara
katika radio hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kushuto ni Mkurugenzi wa vipindi
kutoka Times Fm Bw. Amani Missana.Picha
na:
Genofeva Matemu - WHUSM
Na Shamimu Nyaki - WHUSM.
Serikali imewataka
waandishi wa Habari na Watangazaji kutumia lugha ya Kiswahili kwa ufasaha
wanapofikisha ujumbe kwa hadhira na kuzingatia kuwa Kiswahili ndio lugha inayotambulisha
Taifa letu hivyo wanapaswa kutumia lugha hiyo kwa usahihi.
Hayo yamesemwa leo na
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
alipotembelea kituo cha redio cha Times Fm ambapo amewataka waandishi na watangazaji
kuzingatia Utamaduni wa nchi yetu hasa matumizi sahihi ya lugha ya Kiswahili
ili kukitangaza na kukiendeleza kama adhma ya Serikali inavyosema.
“Nyie ni mabalozi wa
lugha yetu ya Kiswahili kwa kuwa mnakitumia kila siku katika kufikisha ujumbe
kwa hadhira yenu hivyo mnapaswa kukitumia kwa ufasaha kuleta maana ambayo
mmeikusudia”. Alisema Mhe. Mwakyembe.
Aidha amewataka
waandishi na watangazaji ambao bado hawakizi vigezo vya kuwa katika tasnia hiyo kwenda shule kuongeza elimu na ujuzi
unaotakiwa katika fani hiyo kabla muda wa ukomo uliotolewa kumalizika
kulingana na Sheria ya Habari ya mwaka
2016 inavyosema.
Akizungumzia Sekta ya
Sanaa na Utamaduni Dkt. Mwakyembe ameeleza kuwa Serikali inaendelea kuandaa
Sera nzuri itakayoleta matokeo chanya kwa wasanii kupitia kazi zao hususani suala
la wizi wa kazi hizo pamoja na kuwa na Hati Miliki ya kazi zao kwa kushirikiana
na COSOTA.
Kwa upande wake Meneja
wa Vipindi wa redio hiyo Bw. Amani Missana amesema kuwa redio hiyo inashiriki
kwa ukamilifu katika kuhamasisha Watanzania kuunga mkono Sera ya Tanzania ya
viwanda kupitia vipindi mbalimbali ikiwemo kipindi cha “Hatua Tatu”
kinachorushwa kila siku za wiki asubuhi.
Hata hivyo
ameishukuru Serikali kwa ushirikiano inaowapatia katika kutekeleza wajibu wao
wa kuwaelimisha na kuwaburudisha wananchi na kuahidi kuendelea kufanya hivyo
kwa uzalendo bila kuvunja Sheria ya kanuni za utangazaji na uandaaji wa vipindi
vyenye kutoa mtazamo chanya kwa
wananchi.
No comments:
Post a Comment