Habari za Punde

Mwenge wa Uhuru Ukiendelea na Mbio Zake na Kuzindua Miradi ya Maendeleo Kisiwani Pemba.

KIONGOZI wa mbio za mwenge wa uhuru, Amour Ahmad Amour, akisalimiana na Mkuu mpya wa wilaya ya Chakechake Rashid Hadid, wakati mwenge huo akikabidhiwa ukitokea wilaya ya Mkoani, ili autembeza wilayani mwake, kwa ufunguzi na uwekaji wa mawe ya msingi kwa miradi mbali mbali ya kimaendeleo
MMOJA ya wakimbiza mwenge wa uhuru, akisalimiana na Mkuu mpya wa wilaya ya Chakechake Rashid Hadid, wakati mwenge huo akikabidhiwa ukitokea wilaya ya Mkoani, ili autembeze wilayani mwake, kwa ufunguzi na uwekaji wa mawe ya msingi kwa miradi mbali mbali ya kimaendeleo
 KATIBU Tawala wilaya ya Mkoani Pemba, Miza Hassan Faki katikati), akisoma risala ya wilaya yake, kwenye hafla ya makabidhiano ya mwenge wa uhuru, kwa ajili ya kutembezwa wilaya ya Chakechake, hafla hiyo ilifanyika skuli ya Ngwachani
VIONGOZI mbali mbali wakiogozwa na Mkuu wa wilaya ya Chakechake Rashid Hadid Rashid, wa mwanzo kulia, wakisikiliza hutuba inayotolewa na Katiba Tawala wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki, hayupo pichani, kabla ya viongozi hao, kukabidhiwa kwa ajili ya kutembezwa wilaya ya Chakechake. 
MKUU wa wilaya ya Mkoani  Hemed Suleiman Abdulla, (kulia), akimkabidhi mwenge wa uhuru Mkuu mpya wa wilaya ya Chakechake, Rashid Hadid Rashid, ili nae autembeze ndani ya wilaya hiyo, baada ya kumaliza mbio hizo wilaya ya Mkoani

KITUO kipya cha afya cha daraja la pili, cha Pujini wilaya ya Chaechake kisiwani Pemba, ambacho tayari kimeshafunguliwa na kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru Amour Ahmad Amour, kwenye shamra shamra hizo, wilayani humo.
 (Picha na Haji Nassor, Pemba).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.