NA HAJI NASSOR, PEMBA
WAZAZI na walezi wilaya ya Chakechake
kisiwani Pemba, wametakiwa kuacha kuwafuga watoto wao na badala yake wawalee,
ili wakuwe katika malezi bora na makuzi, yenye kufuata nyenendo na tamaduni
zenye tija.
Kauli
hiyo imetolewa na Mwalimu Mkuu wa skuli ya Maandalizi ya star ya Kichungwani
Chakechake, Moza Said wakati alipokuwa akizungumza na wanafunzi, wazazi na
walezi kwenye siku ya wazazi na mahafali ya wanafunzi wao, hafla iliofanyika
uwanja wa Tennis.
Alisema,
mfumo wa kuwalea watoto kwa njia ya kuwafuga, na kuwapa kila watakacho na
kuwaacha kufanya kila wajiskiavyo, kunaweza kuwasababishia kujikaribisha na
udhalilishaji ulioshamiri katika siku za hivi karibuni.
Alisema,
ni lazima wazazi na walezi hao, wakaze kamba kwenye kuwalea watoto wao, kwa
mujibu wa tamaduni za kizanzibar zinavyoelekeza maadili na mwenendo mwema.
“Sisi
walezi lazima tutofautishe baina ya kumlea mtoto na kumfuga, maana tukimfuga
basi tutaharabikiwa hapo baadae, lazima tushirikiane kati malezi”,alisema.
Katika
hatua nyengine Mwalimu Mkuu huyo wa skuli ya Maandalizi ya Star, aliwataka
wazazi kuwendelea kushirikiana na uongozi wa skuli hiyo, ili wanafunzi wapate
msukumo wa maisha yao ya kutafuta elimu.
Mapema
aliewahi kuwa Mkuu wa wilaya ha Chakechake Hanuna Ibrahim Massoud, aliwataka
wazazi na walezi, kujitahidi kuwalipia watoto wao ada, ili skuli hiyo isonge
mbele.
Aidha
alisema, uanzishwa wa skuli hiyo, ni kuitikia wito wa serikali wa kuwapatia
elimu bora watoto wanaoanza skuli za Maandalizi, kabla ya kuingia msingi.
Hivyo,
alisema kama wazazi wameamua kuwapeleka watoto wao kwenye skuli hiyo, lazima
waelewa kuwa suala la kulipa ada halina mjadala.
“Mimi
niwataka wazazi wale wazito wa kutoa ada, sasa wajikaze sana maana, mambo
mazuri yalipo Star nasari, pia yanategemea ulipaji wa ada za watoto
wenu”,alifafanua.
Akisoma
risala ya Mwalimu, Hawa Abdalla Mohamed, alisema bado wanakabiliwa na
changamoto kadhaa, ikiwa ni pamoja na kukosa jengo la kuanzisha skuli ya
Misingi.
Jengine,
alimuomba mgeni rasmi, kushughulia uwezekano wa kuwekewa matuta kwenye barabara
yao inayopita chini ya skuli yao, ili kuepusha ajali zisizokuwa za lazima.
“Karibu
na skuli yetu, pana barabara inayoruhusu kupitishwa kwa vyombo vya moto tena kwa
mwendo kasi, sasa kabla hapajatokezea ajali, lishughulikie”,alishauri.
Awali
wanafunzi hao katika skuli ya Maandalizi ya Star, iloanza zaidi ya miaka nane
sasa, walionyesha umahiri wao katika nyimbo, sanaa, tamaduni, kucheza, michezo
ya kuvuta kamba na kupasua mabofu.
No comments:
Post a Comment