Habari za Punde

Utiaji wa saini wa makubaliano ya ushirikiano wa hospitali ya Abdalla Mzee na ya Jiangsu Nanjing ya China

 KIONGOZI mkuu wa madaktari kutoka China wanaotoa huduma za matibabu Hospitali ya rufaa ya Mkoa ya Abdulla Mzee Mkoani Pemba, dk Chen Er Dong, akizungumza kwenye hafla ya kutimia mwaka mmoja wa hospitali hiyo, tokea kufanyiwa matengenezo makubwa, pamoja na utiaji wa saini wa makubaliano ya ushirikiano wa hospitali hiyo na ile ya Jiangsu Nanjing, kwa ajili ya mafunzo ya madaktari wazalendo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 KIONGOZI mkuu wa madaktari kutoka nchini China dk Chen Er Dong, akisaini makubaliano ya ushirikiano wa Hospitali ya rufaa ya Mkoa ya Abdulla Mzee na hospitali ya China ya Jiangsu Nanjing, kwa ajili ya mafunzo, kwa madaktari wazalendo, hafla  iliofanyika jana Mkoani Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 WA pili kulia ni Kiongozi mkuu wa madkatri nane kutoka China, dk Chen Er Dong, akimkabidhili Mkuu wa wilaya ya Mkoani Hemed Suleiman Abdulla, viti 50 kwa ajili ya hospitali hiyo, ambapo wa mwisho kushoto ni Mganga mkuu wa hospitali hiyo, dk Haji Mwita Haji na Katiba tawala wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki, (Picha na HajI Nassor, Pemba) 
 BAADHI ya viti 50 vilivyotolewa na timu ya madaktari nane kutoka China, wanaoendelea kutoa matibabu katika hospitali ya Mkoa ya Abdulla Mzee, ambapo viti hivyo ni kwa ajili ya hospitali hiyo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 MKUU wa wilaya ya Mkoani Pemba, Hemed Suleiman Abdulla, akisalimiana na kiongozi mkuu wa madaktari waliopo hospitali ya Mkoa ya Abdulla Mzee, dk Chen Er Dong, muda mfupi, baada kusaini makubaliano ya ushirikiano kati ya hospitali hiyo na ile ya China ya Jiangsu Ninjing, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
MADAKTARI nane kutoka China, wakiwa kwenye picha ya pamoja, mara baada ya kumalizika kwa hafla ya utilianaji saini juu ya makubaliano ya ushirikiano kati ya hospitali ya Mkoa ya Abdulla Mzee na hospitali ya Jiangsu Ninjing kwa ajili ya mafunzo ya kitabibu na madaktari wazalendo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.