Habari za Punde

KATIBU MKUU WA UVCCM KUZINDUA ALBAM YA MSANII MGEGO TAREHE 30 /09 /2018 MKOANI IRINGA


NA FREDY MGUNDA,IRINGA

KATIBU mkuu wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) taifa kuwa mgeni rasmi katika uzindua albam ya nyimbo za injili ya msanii James Mgego wa mkoani Iringa  inayoitwa “Achani Mungu Aitwe Mungu” na uzinduzi huo utafanyika katika ukumbi wa HIGHLAND HALL uliopo mjini iringa tarehe 30 /09 /2018.

Akizungumzia uzinduzi huo msanii wa nyimbo za injili James Mgego alisema kuwa anatarajia kuzindua albam yenye nyimbo tisa zilizotengenezwa katika studio za Nice zilizopo mkoani Iringa.

Mgego alisema kuwa mgeni rasmi atakuwa katibu mkuu wa umoja wa vijana ndugu Raymond Mwangwala(MNEC) na viongozi wengi wa serikali na wakisiasa kutoka mkoani Iringa na nje ya mkuoa wa Iringa.

Katika uzinduzi huo kutakuwa na kwaya mbalimbali ambazo zitatumbuiza kama vile TAC kwaya Anglicana, Nuru kwaya Anglicana,TAG Mlandege,Mhimidini Mlandege,Kwaya ya vijana kanisa kuu,kwaya mkuu kihesa,uinjilisti KKKT Ipogolo, uinjilisti KKKT PHM frelimo,kwaya ya vijana kitwilu,RC Mshindo,ACT fellowship,Faith kwaya tumain, RC kichangani kihesa,Sayuni Anglican Ipogolo na Elishadai Anglican Ilula.

Aidha Mgego alisema kuwa kutakuwepo na waimbaji maalufu na mashuhuri wa nyimbo za injili ndani na nje ya mkoa wa Iringa watakuwepo kama vile DR Tumaini Msowoya,Nesta Sanga,Ntimiza Rwiza,Samson Kihombo,faraja kigula,Mwl Senje,mama masawe mwamvita,Petro Chetenge,Raymond Mwalisu,Tukuswiga Ikoso na wengine wengi.

Mgego alisema kuwa anawakabiribisha wananchi wote katika uzinduzi huo ambapo hakutakuwa na kiingilio chochote kile.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.