Habari za Punde

Benki ya NMB Yakabidhi Vitanda na Mashuka Hospita ya Mnazi Mmoja Wodi ya Watoto na Wazazi Jengo la Dodoma Zanzibar.


Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud (alievaa tai rangi ya bluu) akimkabidhi  Kitanda na Mashuka Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Mnazimmoja Dkt. Ali Salum (kulia) Mbunge wa viti Maalum Wanawake CCM Asha Abdalla Juma, Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Zanzibar Abdalla Duchi na (kushoto) Meneja Uhusiano Faraja Kaziulaya kutoka Dar es Salam.
Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Zanzibar Abdalla Duchi akimkabidhi Mashuka na Kitanda Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud (kulia) ni Mbunge wa viti Maalum Wanawake CCM Asha Abdalla Juma (Mshua) na Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Mnazimmoja Dkt. Ali Salum.
Mbunge wa viti Maalum Wanawake CCM Asha Abdalla Juma (Mshua) na Mdau wa mambo ya afya akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada wa Vitanda na Mashuka kwaajili ya huduma za Kujifungulia katika Hospitali Kuu ya Mnazimmoja jengo la Dodoma.
Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Zanzibar Abdalla Duchi akizungumza na Mgeni Mwalikwa pamoja na Watendaji wa Hospitali ya Mnazi Mmoja kabla ya kukabidhi msaada wa Vitanda nane (8) na mashuka mia moja na ishirini (120) kwaajili ya Hospitali hiyo.
Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud ambae ni Mgeni Mwalikwa katika hafla ya kukabidhi Vitanda na Mashuka akizungumza machache kabla ya kukabidhiwa msaada huo( kulia) ni Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Zanzibar Abdalla Duchi, Meneja Miradi Benki ya NMB Lilian kisamba na Mbunge wa viti Maalum Wanawake CCM Asha Abdalla Juma (Mshua).
 Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Mnazimmoja Dkt. Ali Salum akitoa shukurani kwa kupokea msaada wa Vitanda na Mashuka uliotolewa na Benki ya NMB katika hafla iliofanyika  katika Haspitali ya Mnazimmoja jengo la Dodoma.
Watendaji wa Hospitali ya Mnazimmoja waliohudhuria katika  hafla ya kukabidhiana msaada wa Vitanda na Mashuka.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.