RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein,
ameondoka nchini leo kuelekea Uingereza kwa safari maalum.
Katika
uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume viongozi mbali mbali wa
Serikali, vyama vya siasa pamoja na wakuu wa vikosi vya ulinzi na usalama wa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud
walimuaga Rais Dk. Shein.
Dk.
Shein katika safari hiyo, amefuatana na Mkewe Mama Mwanamwema Shein pamoja na Watendaji
wengine wa Serikali.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment