Habari za Punde

Utunuku wa Nishani ya Mapinduzi na Uongozi Uliotukuka Zanzibar.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akimtunuku Nishani ya Mapinduzi ya Viongozi Mhe. Mohammed Seif Khatib,hafla hiyo imefanyika leo jioni katika viwanja vya Ikulu Zanzibar jioni hii.  

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein ametunuku Nishani ya Mapinduzi, Nishani ya Utumishi Uliotukuka pamoja na Nishani ya Ushujaa kwa Viongozi, Watumishi wa Umma, Maafisa na Wapiganaji wa Idara za SMZ na wananhi mbali mbali wenye sifa maalum.

Hafla hiyo ilifanyika katika viwanja vya Ikulu mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa vyama vya siasa, Serikali, wananchi pamoja na viongozi wakuu wastaafu akiwemo Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ali Hassan Mwinyi, hafla hiyo ni miongoni mwa shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.

Mapema akitoa tamko la kwanza la kuashiria kuanza shughuli hiyo, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Salum Maulid Salum alisema kuwa Rais Dk. Shein ametunuku Nishani ya Mapinduzi 45, Nishani ya Utumishi Uliotukuka 53 na Nishani ya Ushujaa 14 kwa Viongozi, Watumishi wa Umma, Maafisa na Wapiganaji wa Idara za SMZ na wananhi mbali mbali.

Katibu Salum alieleza kuwa sherehe hiyo ilihudhuriwa na watunukiwa 112 ambao kati ya hao 40 ni Marehemu ambao Nishani zao zimepokelewa na wawakilishi wao na 72 wako hai ambapo nishani zao watapokea wenyewe au zitapokewa kwa niaba yao.

Alisema kuwa Watunuku wote sifa zao zimekidhi matakwa ya Nishani hizo ambapo Nishani ya Mapnduzi hutolewa kwa mtu ambaye aliasisi au alishiriki au aliyatukuza na aliyaenzi Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.

Aliongeza kuwa Mtunukiwa ni pamoja na Kiongozi au mtu mwengine aliyehai au aliyefariki ambaye aliiletea sifa Zanzibar katika fani mbali mbali na kuonesha maadili mema ya kusifika na kuigwa ambapo katika Sherehe hizo, Nishani ya Mapinduzi inatunukiwa katika kundi la Viongozi na Wananchi wenye sifa maalum.

Kwa maelezo ya Katibu Mkuu huyo Nishani ya Utumishi uliotukuka inatolewa kwa Mtumishi wa Umma au Idara Maalum za SMZ aliyehai au aliyefariki ambaye ametimiza Utumishi wake kwa muda wa miaka isiyopungua 20 mfululizo na kwa Mtumishi wa Idara za SMZ miaka isiyopungua 20 ya kuwa Ofisa na katika kipindi chote hicho amekuwa na tabia njema.

Aliongeza kuwa Mtumishi huyo awe ametumikia Taifa kwa Uzalendo wa hali ya juu na kufanya kazi kwa kujitolea, uwajibikaji, uadilifu, ujasiri na umakini katika kusimamia majukumu na utendaji kazi.

Aidha, Katibu Salum alieleza kuwa Nishani ya Ushujaa inatolewa kwa Mtumishi wa Idara Maalum za SMZ au mtu mwengine yoyote aliyehai au aliyefariki ambaye ametenda kitendo cha Ushujaa, Ujasiri na Uzalendo ambacho kimesaidia kuokoa mali au uhai wa mtu au kujitolea maisha yake kwa ajili ya ulinzi wa Taifa.

Pamoja na hayo, Katibu Mkuu huyo alieleza kuwa Vitendo hivyo vya ushujaa viwe wazi ambavyo alivifanya na kuthibitishwa, mahala popote pale penye hatari na ameendelea kuwa muaminifu na mtiifu kwa nchi na Serikali yake.

Nishani zilizotolewa ni pamoja na Nishani ya Mapinduzi kwa Viongozi na wananchi wenye sifa mbali mbali akiwemo CP Ali Abdalla Ali, Balozi Omar Ramadhan Mapuri, Dk. Mohamed Seif Khatib, Said Bakari Jecha na Meja Mstaafu Haji Abdalla Sadala.

Wengine ni Balozi Mohamed Mwinyi Mzale, Abdulrahman Mwinyi Jumbe, Masauni Yussuf Masauni, Abdalla Rashid Abdalla, Msham Abdalla Khamis, Biubwa Amour Zahor, Jogha Shaali Khatib,  Sihaba Ismail Faraghani, Said Rashid Mohamed, Kombo Hassan Juma, Haji wa Haji wa Haji Mohamed Idd Juma, Amina Khamis Borafia.

Rais Dk. Shein pia, amewatunuku Khatib Idd Khatib, Mohamed Yahya Juma, Salum Hassan Mzee, Khamis Amour Mzee, Borafia Silima Juma, Kombo Ali Vuai, Salim Ali Matta, Juma Ali Juma, Marehemu Rashid Mohamed Khamis, Marehemu Haji Kombo Mbaraka, Marehemu Othamna Bakari Othman na  Marehmu Ame Mohamed Juma.

Wengine waliopewa Nishani hizo ni Marehemu Said Mwinyichande Mkanga, Safia Maneno Suleiman, Marehemu Ali Khamis Suleiman (Ali Kima), Marehemu Juma Othman Faki, Marehemu Ramsa Mbarouk Foum, Marehemu Hussein Ayoub Mussa, Marehemu Hassan Faki Kombo na Marehemu Jafari Ali Haji (Suwedi Mabugira), Marehemu Omar Ussi Muhidini na Marehemu Said Mussa Ali.

Aidha, Dk. Shein ametoa Nishani ya Mapinduzi kwa Timu za Mpira na Vikundi vya Uhamasishaji vikiwemo Timu ya Zanzibar Hero 2017, Timu ya Zanzibar ya Mpira wa Ufukweni 2017, Bendi ya Safari Trippers na Kikundi cha Taarab cha Siti Binti Saad.

Pamoja na hayo, Rais Dk. Shein ametoa Nishani ya Utumishi Uliotukuka kwa Watumishi wa Serikali wakiwemo Balozi Hussein Said Khatib, Julius B. Raphael, Salmin Senga Salmin, Dk. Mohamed Saleh Jidawi, Uledi Mwita Kisumku, Khadija Ali Mohamed, Ahmed Himid Mbaye, Tamim Amour Hassan na Said Mohamed Hussein.

Razina Mohamed Salum, Fatma Mohamed Said, Omar Mtawa Khatib, George Hanry Majaaliwa, Theresia John Mwakanjuki, Aziza Hussein Said, Msanif Haji Mussa, Mwaka Ahmed Said, Khamis Juma Zaid (Khamis Leza) na Khamis Juma Khamis.

Pia, Rais Dk. Shein amewatunuku Nishani Ameir Suleiman Haji (Njeketu), Marehemu Mussa Haji Foum, Marehemu Abdulwahab Alawi Abdulwahab, Marehemu Himid Msoma Abdallah, Marehemu Mgeni Mwalim Ali, Marehemu Rahma Mohamed Mshangama, Marehemu Salmin Hafidh Ameir, Marehemu Uled Juma Wadi, Marehemu Mohamed Said Mohamed, Marehemu Dk. Malick Abdalla Juma.

Wengine ni Mwarabu Khalfan Mohamed, Marehemu Shaaban Salum Mohamed, Marehemu Nassor Khatib Pandu, Marehemu Talib Mahadhi Ali, Marehemu Saad Jaffar Ali, Marehemu Dk. Hababuu Mohamed Chwaya, Marehemu Juma Ame  Juma.

Rais Dk. Shein pia, amewatunuku Nishani Marehemu Juma Maalim Vuai, Marehemu Asha Mussa Ahmed, Marehemu Bimkubwa Ali Saleh, Marehemu Said Mohamed Hassan na Marehemu Said Waziri Mshauri.

Aidha, Rais Dk. Shein amewatunuku Nishani ya Utumishi Uliotukuka Watumishi wa Idara Maalum za SMZ ambao ni Kapteni (CAPT) Othman Mwinyi Mzee, Luteni Kanali (LT.COL) Jabir Haji Hamza, Luteni Kanal (LT. COL) Mussa Mohamed Shaame, Luteni Kanali (Jabir Saleh Simba, Senior Assistant Commissioner of Prison (SACP) Juma Omar Kona, Luteni Kamanda (LCDR) Ramadhan Hassan Mzee, Senior Superintendent of Fire (SSF) Ame Ali Suleiman.

Wengie ni Assistant Superintendent of Fire (ASF) Mwanakhamis Hassan Kongwa, Marehemu Commander (CDR) Simai Rajab Kombo na Marehemu Leutninate Commander (LCDR) Juma Abrafman Sadik.

Rais Dk. Shein ametoa  Nishani ya Ushujaa kwa Watumishi wa Idara Maalum za SMZ  akiwemo Mstaafu Luteni Kamnada (LT.CDR) Abdulrahman Mohamed Shamte, Assistant Superintendent of Fire (ASF) Asha Othman Said, Assistant Inspector of Fire (A/INSF) Ali Makame Ali, Assistant Inspector of Prison (A/INSP) Msim Said Mzee, Master Chief Petty Office (MCPO) Ali Bakari Haji.

Wengine ni Segeant (SGT) Ali Omar Abdalla,Segeant (SGT) Said Abdalla Abeid, Segeant (SGT) Kombo Salum Kombo, Segeant (SGT) Mwanaisha Kayamba Khamis, Fireman (F/M) Mohammed Shaaban Khamis, Marehemu Sea One (S/1) Masoud Peya Yussuf na Marehemu Sub Liutenant (SUB/LT) Mfaume Ali Juma.

Pia, ametunuku Nishani ya Ushujaa kwa Ali Ameir Mwalim aliyejitolea kupiga mbizi katika pango la maji kwa ajili ya kuchukua sampuli za mchanga ili kuweza kupata wingi wa maji na hatimae kumepatikana kisima cha maji ambayo wananchi wanatumia hadi hivi leo katika eneo la Dimani mnamo miaka ya 1960. Shujaa mwengine ni Muhamad Haji Muhamad aliyeokoa maisha ya mwananchi aliyeingia kisimani katika Shehia ya Kiongoni Makunduchi mnamo mwaka 2018.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.