Wakili Mkuu wa
Serikali, Dkt. Clement Mashamba, akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari(
hawapo pichani) kabla ya kukabidhiwa Mfumo wa Usimamazi wa Mashauri
uliotengenezwa na Wakala ya Serikali Mtandao (e GA), Makabidhiano ambayo yalifanyika
leo Ijuma, Juni 7,2019 Jijini Dar es
Salaam, Kulia ni Mkurugenzi wa Ubora na Udhibiti Mashauri kutoka Ofisi ya
Wakili Mkuu wa Serikali na kushoto ni Mkurugenzi wa Usimamizi wa Huduma za
TEHAMA wa Wakala ya Serikali Mtandao, Injinia Benedict Ndomba.
Wakili Mkuu wa
Serikali, Dkt. Clement Mashamba(Kulia), akipokea rasmi Mfumo wa Usimamazi wa
Mashauri kutoka kwa Mkurugenzi wa Usimamizi wa Huduma za TEHAMA wa Wakala ya
Serikali Mtandao, Injinia Benedict Ndomba(Kushoto) Makabidhiano hayo yalifanyika leo Ijuma, Juni 7,2019
Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Usimamizi wa Huduma za TEHAMA wa
Wakala ya Serikali Mtandao, Injinia Benedict Ndomba (wa kwanza kushoto) akitoa
maelezo kuhusu ufanyaji kazi wa Mfumo wa Usimamazi wa Mashauri
uliotengenezwa na Wakala ya Serikali Mtandao (e GA) mbele ya Wakili Mkuu wa
Serikali, Dkt. Clement Mashamba( wa pili kushoto) katika makabidhiano ya Mfumo
huo mapema Leo Jijini Dar es Salaam.
Na.Paschal
Dotto-MAELEZO.
Serikali Kupitia
Wakala ya Mtandao (e GA) imekabidhi rasmi Mfumo wa Taarifa wa Usimamizi
Mashauri, kwa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali ili kuiwezesha Ofisi hiyo
Kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi Mkubwa.
Akizungumza ya
Waandishi wa Habari katika makabidhiano kati ya Wakala ya Serikali ya Mtandao
na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Mkurugenzi Wa Usimamizi wa Huduma za
TEHAMA wa Wakala ya Serikali, Injinia, Benedict Ndomba, amesema kuwa Ofisi yake
inatumia wataalam wake wa TEHAMA kutengeneza mifumo inayorahisisha kufanya kazi
katika Taasisi mbalimbali nchini.
Injinia Ndomba,
alisema kuwa serikali ya Awamu ya Tano inalo kusudi kubwa la kutekeleza ahadi
zake kama utoaji huduma nzuri kwa wananchi ikiwemo hiyo ya utengenezaji mifumo
ya huduma kwa ajili ya kero za wananchi.
“Serikali hii ya
Awamu ya Tano, ina hazina kubwa ya wataalam wa TEHAMA, ambapo kielelezo kimojawapo
ni kuwa mfumo huu umebuniwa, umesanifiwa na kutengenezwa na Watumishi wa Umma
na tumekubaliana na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kuwa Mfumo huu utekelezwe
kwa awamu mbili ili kuweza kukidhi mahitaji ya wadau wote”, Injinia Ndomba
alisema.
Katika awamu ya
Kwanza ya Utengenezaji Mfumo huo, Ndomba alisema wametengeneza Moduli
itakayoisaidia Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kutekeleza majukumu yao hasa ya
ndani kwenye masuala ya Usimamizi Mashauri, ambapo pia itakuwa ni nyenzo muhimu
wa utekelezaji majukumu kwa haraka.
Naye, Wakili Mkuu wa
Serikali, Dkt. Clement Mashamba ameipongeza
Wakala ya Mtandao wa Serikali (e GA) kwa kutengeneza mfumo huo kwa mahitaji ya
ofisi ya Wakili wa Serikali na kudai kuwa watakuwa wanatekeleza majukumu kwa
haraka na kwa ufanisi zaidi katika kutatua kero za wananchi.
“Ofisi yangu
itaendelea kushirikiana na Wakala ya Serikali ya Mtandao ili kuhakikisha awamu
zote za utengenezaji wa mfumo huu zinatekelezwa kwa wakati na kwa ubora
unaostahili, lakini pia Ofisi yangu inatambua Mchango huu mkubwa kwa kazi zetu
ya kisheria,” Dkt. Mashamba.
Aidha Dkt. Mashamba
alisema kuwa mfumo huo utakuwa ni muhimu katika kutatua kero za wananchi, hususani
Usimamizi wa majalada ya Mashauri; Usajili wa Mashauri; Upangaji wa Mashauri
yanayoshughulikiwa; Ufutiliaji wa Maendeleo ya Mashauri; Huduma zingine ni
Usimamizi wa Ratiba ya Mashauri; Utoaji wa Taarifa; Uhakiki wa Mwenendo wa
Mashauri na Uhamishaji wa Taarifa na Takwimu.
Dkt. Mashamba
alieleza kuwa mfumo huo una umuhimu mkubwa kwani unaweza kutumiwa na idara
mbalimbali za Serikali na unapatikana mahali pamoja kwa hiyo ni mfumo ambao
Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali itaweza kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa.
No comments:
Post a Comment