Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, wakati wa mkutano wa Utekelezaji wa Bajeti na Mpango Kazi kwa mwezi wa Julai 2018 hadi Juni 2019, kwa Wizara hiyo uliofanyika ukumbi wa Ikulu Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk. Ali Mohamed Shein ametoa pongezi kwa uongozi wa Wizara ya Elimu na kueleza juhudi za makusudi zilizochukuliwa na Serikali katika kuhakikisha Bajeti ya Wizara yake zinaimarika ikiwemo Wizara hiyo ili kukuza sekta ya elimu nchini.
Hayo aliyasema leo, Ikulu mjini Zanzibar
alipokutana na uongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali wakati ilipowasilisha utekelezaji wa Mpango Kazi wa Julai 2018 hadi Juni 2019 sambamba na Mpango Kazi wa mwaka 2019/2020.
Dk. Shein alitumia fursa hiyo kutoa pongezi zake kwa kutekeleza vyema majukumu ya Wizara hiyo na kuwasilishwa vyema Mpango Kazi
wake huku akisisitiza kuyatangaza mafanikio yaliopatikana katika Wizara hiyo.
Aidha, alieleza mafanikio yaliofikiwa katika kuendeleza na kukiimarisha
Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA),
ambacho amesema hivi sasa kinatambulika duniani kote kutokana na mafanikio yaliopatikana na hatimae elimu imeimarika hapa
Zanzibar.
Rais Dk. Shein aliongeza kuwa Chuo Kikuu hicho cha
SUZA kimepata usajili kamili,
huku hospitali ya Mnazi Mmoja nayo imepata hadhi ya kuwa hospitali ya mafunzo na kupata cheti maalum
cha utambulisho.
Nae Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi
Dk.
Abdulhamid Yahya Mzee aliipongeza kazi nzuri ya uwasilishaji iliyofanywa na Wizara hiyo na kusisitiza kuimarishwa kwa mashirikiano kati ya uongozi na wafanyakazi wa Wizara hiyo.
Mapema Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe.Riziki Pembe Juma katika taarifa yake alieleza utekelezaji wa malengo na vipaumbele ambavyo miongoni mwao ni ujenzi wa jengo jipya
la Taasisi ya Karume ya sayansi na Teknolojia ambao umekamilika na Taasisi ya Maendeleo ya Utalii unaendelea na umefikia asilimia
90.
Aidha, alieleza kuwa ujenzi wa vituo vya Amali Daya na Makunduchi unaendelea vizuri ambapo ujenzi wa kituo
cha Daya umefikia asilimia 65 na Makunduchi umefikia asilimia 55, pia,
alieleza maendeleo ya ujenzi wa skuli mbali mbali za Unguja na Pemba.
Hivyo, Rais Dk.
Shein alisisitiza haja ya kuengeza kasi katika ujenzi wa vituo vya amali vya Daya na Makunduchi ili kufikia malengo yaliyokusudiwa ikiwa ni pamoja na kumaliza kwa wakati uliokusudiwa.
Alieleza kuwa utoaji wa chakula kwa wanafunzi wa Skuli 27
za Msingi unaendelea Unguja na Pemba ambapo pia, jumla ya vituo 20 vya TUTU
vimepatiwa jumla ya TZS 242,250,000
ikiwa ni fedha za ruzuku za kuendeshea vituo na skuli hizo.
Sambamba na hayo, Waziri Pembe alieleza kuwa jumla ya wanafunzi
1,720 wapya walipatiwa mikopo wakiwemo 1475 wa vyuo vya ndani na 245 kwa vyuo vya nje ya
Tanzania huku akieleza kuwa Chuo cha Kilimo cha Kizimbani kimeunganishwa rasmina
Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar mnamo Juni 24, 2019.
Pamoja na hayo,
Waziri huyo alieleza baadhi ya changamoto zinazoikabili Wizara hiyo ambazo hata hivyo juhudi za makusudi zinaendelea kuchukuliwa na serikali kwa lengo
la kuzitafutia ufumbuzi.
Mshauri wa Rais Pemba Dk.
Mauwa Abeid Daftari alisisitiza haja kwa Wizara hiyo kuyatangaza mafanikio yaliyopatikana katika Wizara hiyo kwani imefanya
mambo makubwa huku akiipongeza Wizara hiyo kwa uwasilishaji wa Mpango Kazi wao huo.
Nae Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dk. Idrissa Muslim Hija alieleza Mpango Kazi wa Wizara hiyo huku akitumia fursa hiyo kumpongeza Rais
Dk. Shein kwa uongozi wake
na kuipongeza Serikali kwa kuipa fedha za kutosha Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali huku akipongeza mashirikiano kutoka kwa wafanyakazi wa Wizara hiyo.
Aidha, aliahidi kulifanyia kazi suala la wanafunziwa
Zanzibar wanaosoma nje ya Zanzibar ambao huja nchini kufanya tafiti mbali mbali kwa lengo
la kuwasaidia ili kutekeleza vyema zoezi lao hilo.
Aidha, kwa upande wa Skauti uongozi wa Wizara hiyo ulieleza azma ya kuwarejesha vijana kuwa na maadili na uzalendo ikiwa ni pamoja na kurejesha na kuanza vikundi vya Skauti katika skuli za
Zanzibar.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment