KIJANA Ali Khamis Abdalla akiwa nje ya gari yake baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika bonanza la Utalii, lililofikia tamati katika fukwe za Vumawimbi Wilaya ya Micheweni.
KIJANA Ali Khamis Abdalla akiwa ambaye ni mshindi wa kwanza katika bonanza la utalii Pemba
KIJANA Ali Khamis Abdalla (Wanne katika picha) Kutoka Tumbe Wilaya ya Micheweni, ambaye ameweza kujinyakulia Gari yenye Thamani ya Milioni 7 baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika mashindano ya Traithoni, ikiwa ni bonanza la Tatu utalii Kisiwani Pemba.
GARI ambayo amekabidhiwa bingwa wa bonza la utalii Kiswani Pemba
(Picha na Abdi Suleiman - Pemba.)
Na.Abdi Suleiman na Said Abdulrahman -Pemba.
TAMASHA la tatu la Utalii na
Michezo Kisiwani Pemba, limefikia tamati kwa michezo mbali mbali ikiwemo trithon, mchezo wa kuogolea na resi za ngalawa, huko katika
fukwe za vumawimbi wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kusini Pemba.
Mtamasha hilo liliweza kuvuta hisia za mashabiki wengi katika
kisiwa hicho, hali iliyopelekea kuujaza ufukwe wa vumawimbi, huku
likiwashirikisha wanamichezo wapatao 500 kutoka Zanzibar na Tanzania bara.
Baadhi ya wananchi wa wilaya ya micheweni walishindwa kuzuwia
hisia zao, baada ya kumuona kijana wao Ali Khamis Abdalla kutoka Tumbe,
kuongoza katika mbio za baskeli na kujinyakulia gari, huku wakishindwa kuamini
kilichotokea.
Tamasha hilo ambalo limefungwa na Naibu Spika wa Baraza la
Wawakilishi Zanzibar, Mgeni Hassan Juma, ambapo washindi mbali mbali waliweza
kuzawadiwa zawadi
Washindi hao waliweza kuzawadi mbali mbali zikiwemo fedha
taslimu, baskeli, Honda aina ya boxer na sunlj, huku mshindi wa mashindano hayo
akijinyakulia Gari.
Kwa upande wa michezo ambayo ilishindaniwa na kutolewa zawadi
katika ufungaji huo, ni pamoja na resi za baskeli, mpira wa miguu, resi za
ngawala, uogeleaji, dufu pamoja na mbio za trithon.
Kwa upande mbio za trithon ambazo ziliwashirikisha vijana kutoka
Unguja na Pemba, zikiwashirikisha washiriki 51, ambapo mshindi wa Kwanza ni kijana
Ali Khamis Abdalla kutoka Tumbe Wilaya ya Micheweni, alijinyakulia gari aina
Vtz pamoja na kikombe.
Mshindi wa pili wa mbio hizo ni Khamis Juma Khamis kutoka Dimani
Unguja, ambapo yeye alijinyakulia Honda huku nafasi ya tatu ilichukuliwa na
kijana Hassan Ame Tajo kutoka Dimani nae akajinyakulia Honda aina boxer, huku
washiriki 10 wa mwanzo wakiahidiwa kila mmoja kuzawadiwa shilingi 50,000/.
Kwa upande upigaji dufu, mshindi wa Kwanza kilikuwa ni chuo Cha
Almadrasatul Nurul-Islamiyya kutoka Micheweni ambapo kimejinyakulia kitita Cha
shilingi 3000,000/ taslimu, nafasi ya pili ikichukuliwa na Almadrasatul Munir
Islamiyya kutoka Kangani Mkoani Pemba ambapo nacho kikajinyakulia kitita Cha
shilingi 2000,000/ huku nafasi ya tatu ilichukuliwa na Almadrasatul Thamaratul
Jannar ya Fundo ikajipatia shilingi 1000,000/ huku walimu wa madrasa hizo
walizawadiwa baskeli kila mmoja.
Kwa upande wa Mashindano ya uogeleaji mshindi wa Kwanza alikuwa
ni Hamad Mattar Abdalla ambae alijinyakulia kitita Cha shilingi 1000,000/
pamoja na kikombe, mshindi wa pili ni Faki Omar Faki nae akajinyakulia shilingi
700,000/ na mshindi wa tatu alikuwa ni Ali Hamad Shaame akijichukulia kitita
Cha shilingi 500,000/, ambapo katika mchezo huo waogoleaji wapatao 71
walishiriki Mashindano hayo.
Ama kwa upande resi za ngalawa zilizoshirikisha ngalawa 12,
nafasi ya kwanza ikichukuliwa na Simba Salim Issa kutoka Mnarani Makangale
ambae alijipatia kitita Cha shilingi 1000,000/ na kikombe, nafasi ya pili
ikichukuliwa na Said Khamis Rashid alijipatia kitita Cha shilingi 700,000/ na
mshindi wa tatu ni Ali Shaame kutoka Mnarani akajinyakulia shilingi 500,000/
huku washiriki waliosalia wakiahidiwa shilingi 100,000/.
Kwa upande wa mbio za marathon upande wa wanaume nafasi ya
kwanza ilichukuliwa na kijana Nelson Mbuya kutoka JKU ambae alijipatia kitita
Cha shilingi 800,000/, nafasi ya pili ikachukuliwa na Ali Malik Mohammed na
kujinyakulia shilingi 700,000/ na nafasi ya tatu ilichukuliwa na Mohammed
Ramadhani Mgeni kutoka KMKM ambae alijipatia kitita Cha shilingi 400,000/.
Kwa wanawake ambapo washiriki walikuwa ni wawili tu mshindi wa
Kwanza alikuwa ni Rosemary Gusta kutoka KMKM, ambae alijipatia kitita Cha
shilingi 400,000/, huku nafasi iliyosalia ikichukuliwa na Asha Abdalla Khatib
ambae na akipata shilingi 300,000/.
Kwa upande wa mchezo wa mpira wa miguu ambayo ilishirikisha
vilabu 8 vya mchezo huo, mshindi ilikuwa ni timu ya Mwenge kutoka Wete, ilijipatia
kikombe pamoja na fedha taslim shilingi 3000,000/, mshindi wa pili akizawadiwa
fedha taslim shilingi 2000,000/, huku vilabu vilivyobakia wakiahidiwa mipira ya
kuchezea kila timu.
Akitoa nasaha zake Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar,
Mgeni Hassan Juma, alisema Zanzibar ilikuwa
na ndoto ya kuanzisha mashindano ya trithon jambo ambalo sasa limetimia kwa
upande wa Kisiwa Cha Pemba.
Alisema kufanyikwa mashindano hayo ni kielelezo tosha cha kuibua
vipaji vya wachezaji mbali mbali ya vijana, hali ambayo inaweza kuhamasisha vijana
kujiingiza katika sekta ya utalii.
“Kwa sasa michezo ni ajira na imekuwa ikiajiri vijana wengi na
kutoka sehemu mbali mbali duniani, hivyo vijana kutumia nafasi hii ya michezo
kujitangaza kwenu”alisema.
Tamasha hilo ambalo lilifunguliwa rasmi na Rais Mtaafu wa awamu
ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Ali Hassan Mwinyi mwishoni mwa
wiki iliyopita, ambapo hapo Jana limefungwa na Naibu Spika wa Baraza la
Wawakilishi Mgeni Hassan Juma, michezo mbali mbali iliweza kufanyika.
No comments:
Post a Comment