Na Raya Hamad - WKS
Ø Wananchi waridhishwa na utaratibu
Ø Wasema
ni hatua muafaka kukomesha udhalilishaji
HATUA
ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ya kuanzisha Utaratibu wa Utoaji wa Huduma za
Msaada wa Kisheria na Kurahisisha Upatikanaji wa Haki kwa wenye mahitaji imepokelewa
kwa mikono miwili na wananchi walio wengi, hasa wale wanyonge ambao hali zao za
kipato ni duni au wenye uelewa mdogo wa taaluma ya masuala ya sheria.
Hali
hiyo imebainika muda mfupi tangu Serikali kupitisha na kuanza kutekeleza Sheria
ya Msaada wa Kisheria, iliyowezesha
kuanzishwa Idara ya Msaada wa Kisheria, iliyo chini ya Wizara ya Katiba na
Sheria, ambapo wananchi wengi wameizungumzia hatua hiyo kuwa ni msaada mkubwa
na wa kipekee kwa wananchi walio wengi Unguja na Pemba.
Zuwena
Othman mkaazi wa Bumbwini Makoba anaielezea hatua ya kuanzishwa msaada wa
kisheria na upatikanaji wa haki kwa wale wasiokuwa na uwezo imekuja katika
wakati muafaka ambapo jamii imebadilika kwa kuongezeka watu wasiokuwa na huruma
wala imani kwa wengine.
Zuwena
anasema hivi sasa sehemu zote iwe mjini au vijijini watu wengi wamekuwa wajanja
na kuna matukio mengi ya watu kudhulumiwa na wanaoathirika zaidi ni wale wasiokuwa
na kitu, elimu au watu wakuwasimamia kuweza kupigania haki zao mbele ya Mahakama
na vyombo vyengine vya kutoa haki.
“Kwa
hatua hii Serikali imefanya jambo zuri na la maana… Ni mambo ya kawaida sasa kujitokeza
wajanja kuwahadaa wanyonge kuwaibia ardhi
nyumba, na hata baadhi ya wanaume kwa mfano kwa kujiona wana nguvu hutelekeza
familia na kuwaacha watoto katika shida kubwa wakijua mwanamke hana
pakukimbilia”, alisema Zuwena.
Kwa
mtazamo wake iwapo Serikali itakuwa na utaratibu mzuri wa kuwawezesha wananachi
wasiokuwa na uwezo au ndio walengwa wa msaada huo, kuweza kuwafikia watoaji wa
huduma hizo, hata hivyo vitendo vya watu kudhulumiana kwa njia za hadaa
vitapungua kwa kiasi kikubwa.
Kwa
mujibu wa Sheria hiyo inayojuilikana kama Sheria ya Msaada wa Kisheria ya 2018,
huduma za kisheria zinazotolewa ni utoaji wa ushauri, msaada wa uwakilishi wa
kisheria na taarifa ambapo watakaonufaika ni watu ambao hawana uwezo wa kulipia
huduma hizo za kisheria
Hatua
za utoaji huduma hizo zimeanza baada ya kuundwa Idara ya Msaada wa Kisheria na Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe Dkt Ali Mohamed Shein kwa kumteuwa
Bi Hanifa Ramadhan Said kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Msaada wa Kisheria
Idara ambayo inatekeleza majukumu yake kwa
mashirikiano ya hali ya juu na taasisi mbali mbali za Umma zikiwemo Mahakama,
Polisi na Chuo cha Mafunzo, vile vile, Idara inafanya mashirikiano makubwa na
watoaji wa huduma za msaada wa kisheria na watu binafsi.
Mara
baada ya kuundwa kwa Idara, utekelezaji wa majukumu yake umeanza kwa uzinduzi
rasmi wa Idara hio ambapo uliwakutanisha baadhi ya watoa huduma za Msaada wa
Kisheria pamoja na wanufaika wa huduma za msaada wa kisheria.
Katika
uzinduzi huo Mkurugenzi Hanifa amesema kuwa uwepo wa Idara ya Msaada wa
Kisheria Zanzibar ni kufungua ukurasa mpya katika kuhakikisha kuanzisha haki na
wajibu kwa watoaji wa msaada wa huduma za kisheria kwa vigezo na viwango ili
kwenda sambamba na vigezo vya kimataifa vya utoaji wa msaada wa kisheria.
Anabainisha na kusema kuwa Katiba yetu ya
Zanzibar ya mwaka 1984 inatambua na inahakikisha haki na inajumuisha suala la
msaada wa kisheria kama msingi wa haki za binadamu kwa watu wote. Hivyo, ni
wajibu wa watoaji wa msaada wa kisheria kuifuata miongozo ili kuweza kuisaidia
jamii kupata msaada wa kisheria kwa ufanisi na kwa wakati.
“Niwaombe
kama Watoa huduma za msaada wa kisheria msiishie hapa na juhudi zenu ambazo
mmekuwa mkizifanya kwa muda wa siku nyingi, na muendelee na moyo huo huo katika
kuwajengea uwezo wananchi katika kufahamu haki zao za msingi na wanapata huduma
ipasavyo”. Alisisitiza Hanifa
Mkurugenzi
Hanifa amesema Idara ya Msaada wa Kisheria inathamini kazi kubwa inayofanywa na
Wasaidizi wetu wa Kisheria na watoa huduma wengine wa msaada wa kisheria katika
nchi.
Pia
ametoa shukrani za dhati kwa Jeshi la Polisi kwa kazi ya utoaji wa msaada wa
kisheria kupitia madawati ya kijinsia na njia nyengine ambazo zinasaidia kwa
namana moja au nyengine kusaidia jamii.
Aidha, amewataka watoa huduma za Msaada
wa Kisheria kuendeleza mashirikiano na kuahidi kuitunza Idara na kutekeleza kwa
vitendo Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa ustawi bora katika kuhakikisha kila
mtu anaestahiki kupata msaada wa kisheria anapata kwa kiwango kilicho bora na
kwa wakati.
Sheria
hiyo inazingatia maadili ya jamii na taratibu za kulinda faragha ya mtu wakati
wa kumsaidia kupata huduma za kisheria na haki nyenginezo, ambapo imeeleza kuwa
watu wenye kupatiwa huduma hizo watapatiwa kwa mazingira ya usiri.
Ikizingatiwa
kuwa miongoni mwa wateja watakaoweza kupatiwa huduma hizo ni makundi maalum, wakiwemo
watoto, mayatima, wazee, watu wenye kuishi na virusi vya ukimwi, mambo
yanayohusu migogoro ya ardhi, urithi, unyanyasaji wa kijinsia, uangalizi na
huduma za watoto pamoja na masuala ya uvunjifu wa haki za binaadamu
Sheria
hii inakuja wakati Zanzibar ikikabiliwa na changamoto ya kukithiri kwa vitendo
vya udhalilishwaji watoto, wanawake, watu wenye ulemavu pamoja na wimbi la
talaka linalosababisha watoto kuingia katika mtihani mkubwa kimalezi, ambapo
mara nyingi wazazi wa upande mmoja wa mwanamke ndiye anayebeba jukumu la ulezi
na matunzo.
Ashura
Suleiman mkaazi wa Kijichi Unguja, kwa maoni yake kuja kwa sheria hiyo kutawapa
ahueni baadhi ya wazazi na wana familia ambao watoto wao hasa wasichana wadogo
hupatiwa ujauzito na kukatiwa ndoto zao za kimaisha, huku wazazi hao wakipewa
ushauri mbaya na baadhi ya wanajamii au mara nyengine hata wasijue la kufanya.
“Kuja
kwa sheria hiyo ya msaada wa Kisheria itakuwa ni kimbilio la wazazi na familia
zilizokumbwa na masahiba ya kudhalilishiwa watoto au wanafamilia, huko wataweza
kusaidiwa na kushauriwa vizuri na kujua la kufanya lenye faida kwao”, alisema.
Katika
kufanikisha utoaji wa huduma za kisheria kwa ufanisi wa hali ya juu umewekwa
utaratibu maalum kwa watoaji wa msaada huo, ikiwemo taasisi au mtu anayetoa
huduma hizo kuhakikishwa uwezo wake wa kufanikisha kazi hiyo, ili kuepuka
ubabaishaji na utoaji wa huduma muafaka.
Kwa
maana hiyo sheria hiyo inahitaji mtu, jumuiya au taasisi hiyo kwanza isajiliwe
rasmi na Idara ya Msaada wa Kisheria, ambapo walioanishwa kuwa watakuwa watoaji
wa huduma hizo ni pamoja na Mawakili, Wanasheria, Mavakili pamoja na wasaidizi
wa sheria.
Bila
shaka hatua hiyo imechukuliwa kuhakikisha kwamba wanaotoa huduma za kisheria na
haki kwa wananchi ni watu wenye weledi na uzoefu usionashaka yoyote, hasa
ikizingatiwa kuwa baadhi ya watu wamekuwa na tabia ya kujivisha sifa za
kitaaluma au kazi ambazo hawajazisomea au kuzifanya, lengo lao likiwa ni
kujipatia vipato kwa njia ya udanganyifu.
Sheria
hiyo ya Msaada wa Kisheria na inayorahisisha upatikanaji wa Haki imeliona hilo,
na kuchukua hatua za kudhibiti hali hiyo isitokee, ambapo kwa mujibu wa sheria
hiyo, mtu yoyote ambaye atafanya kazi kama mtoa msaada wa kisheria bila ya
cheti cha usajili kinachotolewa na Mkurugenzi au kujifanya kama mtoa msaada wa
kisheria wakati cheti cha usajili kimesitishwa au kwa makusudi kumzuia mtu
asiombe msaada wa kisheria atakuwa anatenda kosa kisheria
Waziri
wa Katiba na Sheria Mhe Khamis Juma Mwalim katika kikao kilichopita wakati akiwasilisha
bajeti ya Wizara hio alisema kuwa Wizara imejipanga na imefanya ziara ya mafunzo
kuhusu Msaada wa Kisheria na kuwapatia vitendea kazi ili watekeleze majukumu
yao kwa ufanisi.
Hivyo
Waziri Khamis amewaomba watoaji wa huduma za msaada wa kisheria nchini na
wanufaika wa msaada wa kisheria kuielewa vizuri na kuipa ushirikiano Idara mpya
ya huduma za msaada wa kisheria ili kuhakikisha wanawasaidia wananchi wa taifa
hili kuweza kupata haki zao kama ilivyokusudiwa.
Kwa
upande wake, Hamduni Makame ambaye ni mkaazi wa Machui Wilaya ya Kati Unguja,
akizungumzia utaratibu huo wa kuwasaidia kisheria wanaanchi wasiokuwa na uwezo
anasema kuwa kwa hatua hiyo Serikali inastahili kupongezwa kwa sababu wamo
wananchi wengi wanyonge wenye vilio vya muda mrefu, lakini hawana pa kuvipeleka
kutokana na unyonge wao.
Ameeleza
kuwa jambo la muhimu kwa Taasisi inayohusika na Utoaji wa Huduma za Msaada wa
Kisheria kuhakikisha wasiokuwa na uwezo ndio wanaonufaika na utaratibu huo.
Hivyo, ameomba kufanywa kila liwezekanalo kuwazuia wale wenye uwezo wa
kujisimamia na kuendesha kesi na kupata haki zao wenyewe kutoingia katika
utaratibu huo na kuwazuia walengwa.
“Wapo
wajanja ambao wana uwezo mkubwa lakini hujiigiza na kujipatia huduma ambazo
wahawastahili na hivyo kuwazuia wale wanaostahili kupata huduma hizo. Kwa kuwa
Serikali imedhamiria kuwasaidia wasiokuwa na uwezo wa kusimamia haki zao mbele
ya sheria ni matumaini yangu kwamba wajanja hao hawatapewa nafasi”, alisema
Makame.
Amesema
kwamba wamo wananchi wengi ambao uwezo wao na mwamko wa kupigania haki zao ni
mdogo, huku baadhi ya wananchi hao wanashindwa na hata nauli ya kuwawezesha
kufika mahakamani, hivyo uamuzi huo ni jambo la kupongezwa kwa sababu umelenga
hasa kuwakomboa wenye mahitaji.
Katibu Mkuu Wizara ya
Katiba na Sheria Zanzibar ndugu George Joseph Kazi anasema kuwa jamii ielewe kuwa azma ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
nikuahakikisha wananchi wote wanapata huduma stahiki za msaada wa sheria kutoka
kwa watoaji wa huduma za msaada wa kisheria ambao wanasifa zinazoitajika kwa mujibu wa sheria
“tulifanikiwa
kupata Sera ya Msaada wa Kisheria kutokana na jitahada kubwa ya Serikali yetu
kwa kushirikiana na wahusika mbali mbali wa maendeleo na mkiwemo na nyinyi
watoaji wa huduma za msaada wa Kisheria. Hatimae mwaka 2018 tuliweza kupata Sheria
na mwezi Agosti, 2019 tulipata Kanuni za Msaada wa Kisheria zilizotangazwa
Rasmi katika Gazeti la Serikali na kupelekea watoaji wa huduma ya msaada wa
kutambulika rasmi.
George
amewasisitiza watendaji wa Idara ya Msaada wa Kisheria kuwa waadilifu wakati
wakitekeleza wajibu wao na kukumbushia majukumu yao kuwa ni kutoa miongozo ya
kisera kwa watoaji wa msaada wa kisheria, kusajili watoaji wa msaada wa
kisheria, kumtaka mtoa msaada wa kisheria kutoa huduma ya msaada wa kisheria
kwa mtu asiekuwa na uwezo
Pia Kuratibu, kufuatilia na
kutathmini kazi za watoaji wa msaada wa kisheria na kutoa maelekezo ya jumla ya
utekelezaji unaofaa wa program za msaada wa kisheria katika kiwango
kilichowekwa na ubora wa huduma za msaada wa kisheria na Kumshauri Waziri
kuhusu sera na mambo mengine muhimu yanayohusu kuimarisha utaoaji wa msaada wa
kisheria.
Katibu George ameongeza kusema kuwa
Idara ijikite zaidi katika kufanya tathmini na kuandaa taarifa za ufatiliaji na
tathmini ya masuala ya msaada wa kisheria ikiwa ni pamoja na kufanya tafiti ya
changamoto za utoaji na upatikanaji wa huduma za msaada wa kisheria.
Ni
wakati muafaka sasa kwa watoaji wa huduma wa msaada wa kisheria kuzielewa
vizuri kanuni kwa lengo la kuweza kufikisha elimu kwa walengwa ambao ni wataka
huduma wa msaada wa kisheria huku
ikizingatiwa kuwa Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar kupitia Wizara ya Katiba na Sheria Zanzibar imefanikiwa kuwana miongozo mbali mbali
ikiwemo Sera, Sheria, Kanuni na Mpango wa Utekelezaji inayosimamia sekta nzima
ya msaada wa Kisheria.
Kwa
kufahamu kuwa kwa miaka mingi iliopita kwa upande wa Zanzibar kulikuwa hakuna
mfumo rasmi wa kitaasisi unaosimamia huduma za msaada wa kisheria hivyo
kulikosekana Sera au Sheria ambayo ingeweza kusimamia vizuri na kwa ufanisi
huduma za msaada wa Sheria.
Kila mmoja atimize wajibu wake
katika kuhakikisha jamii inapata msaada wa kisheria ili tuwe na jamii yenye
kuelewa sheria na kuweza kudumisha utawala wa sheria, watowaji wa msaada wa
kisheria hawana budi kuipa mashirikiano Idara hii ili iweze kufikia malengo
yake hatua ambayo ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi.
No comments:
Post a Comment