Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Haarrison Mwakyembe akizungumza na
washiriki wa Jukwaa la Waandishi wa Habari Wanawake kuhusu unyanyasaji wa
Kijinsia kwenye vyombo vya habari,
lilifanyika Jijini Dar es Salaam
Na. Judith Mhina -Maelezo
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa
na Michezo Dkt Harrisom Mwakyembe amezindua kitabu cha Gender and Media Handbook in Tanzania wakati wa maadhimisho
ya miaka miwili ya Mtandao wa
Wanahabari Wananawake Tanzania na
Maafisa Uhusiano.
Akizindua kitabu hicho katika
ukumbi wa Kibo ndani ya hoteli i ya
Kimataifa ya Hyatt Regence - The Kilimanjaro leo
Jijini Dar-es-salaam Waziri Dkt Mwakyembe amesema “Wana habari mtakuwa vibarua mpaka lini”.
Hebu tujaribu kutekeleza sheria
mbili ya Habari na ile ya haki ya kupata taarifa, ambapo Tanzania ni kati ya nchi
chache ambazo zimeiga kiila kitu
kilichoandikwa kwenye sheria husika ya kimataifa, badala yake wanaleta mada yao pendwa ya jinsia moja, hatuwezi
kukubali. Amesema Waziri Mwakyembe.
Akijibu risala iliyosomwa na Mwenyekiti wa Mtandao
wa Wanahabari Wananawake Tanzania na Maafisa Uhusiano- Tanzania Women Media and Public
Relation Networ,. Bevin Bhoke Chacha Mwita ambaye amesema kuwa waandishi wa habari wanawalke wananyanyaswa
kijinsia katika vyumba vya habari . Hii ikiwa ni pamoja na kutolipwa mshahara stahiki
kulingana na sifa walizonazo, kutopandishwa madaraja, lugha chafu na kubaguliwa
katika majukumu ya kazi kama waandishi
wa kiume na kujikuta wengi wao
wakiwa waadhirika wa
kunyanyaswa kijinsia.
Waziri mwakyembe aliongeza kwa
kusema “Tunaomba wahisani watenge nusu ya fedha wanazotoa ili kuangalia masilahi ya waandishi wa habari na kuboresha
mazingira ya kazi kutokana na kuwa na vitendea kazi duni katika vyombo vyao vya Habari.
Ninashangaa waandishi wa Habari
ambao wanashangilia kuwa na taaluma isiyo na mpangilio, sheria wala kanuni,
katika kuimarisha taaluma yao na ndio
maana leo hii mnalalamika masilahi madogo
yasiyolingana na kazi mnayofanya
au hatopata mishahara kabisa .
Akisisitiza jambo hilo
Waziri amesema “Ni agfadhali kuwa na
vyombo vya Habari vichache vinavyojali na lulinda masilahi ya Waandishi wa
Habari kuliko kuwa na vyombo vingi ambavyo , haviangalii masilahi ya waandishi
wa Habari, kuwalipa mishahara stahiki kwa wakati .
Akitoa agizo kwa kukabiliana na suala la kupiga vita unyanyasaji
kijinsia Waziri Mwakyembe amesema
kuwa nimefurahi kwa kuwa mmeonyesha namba mbili maalum za simu ambazo yeyote atakayenyanyaswa kijinsia azipige ili
kupata msaada. Aidha, Wizara yangu naiagiza kuwa na namba maalum ya simu ambayo mtanipigia mimi moja kwa
moja na kuwatangaza wale wote
wanaomnyanyasa wanahabari wanawake ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua za
kisheria ili kukomesha vitendo vya unyanyasaji kwenye vyumba vya habari.
Akisisitiza agizo hilo amesema
dirisha la Waziri lipo wazi kwa kila mtu bila mashariti yeyote na naomba
wanahabari walitumie kweli kweli, mimi
nikiwa kama mzazi na kiongozi ni lazima
kuhakikisha suala hili linakuwa historia.
Naye Mwenyekiti wa Mtandao wa wanahabari wanawake na maafisa uhusiano Bi
Chacha ameongeza kwa kusema kuwa
wanawake wana
Katika hizi siku 16 za kupinga
ukatili wa kijinsia katika vyumba vya Habari Mshauri wa masuala
ya wanawake wanahabari Bi Pili Mtambalike amesema “Wanahabari wanawake wananyanyaswa
kijinsia ikiwa ni pamoja na kutengwa kwa kupewa kazi nyepesi ikilinganiswha na waandishi wa kiume katika
vyombo vya habari kutokana na kutokujiamini
Aidha , katika vyombo vingi vya
Habari utafiti unaonyesha kuwa wahariri
wengi ni wa jinsia ya kiume japo wapo
wanawake ambao wanastahili kuwa
wahariri na wanalingana hata kwa taaluma
walizonazo ila hawapewi madaraka na hata hawapandishwi madaraja kama wenzao wa jinsia ya kiume.
Vilevile waandishi
wanahabari wachanga wakike wananyanyaswa kingono
na waliowengi wanafanya kazi kwenye vyombo hivyo kama correspondence na kulipwa kulingana na stori ambayo
haiwatoshelezi kimaisha. Pia, Lugha wanazotumia wahariri katika vyumba vya
habari ni lugha chafu za kudhalilisha na vitisho.
Akiongelea upande wa pili kama
ushauri kwa wanahabari wachanga wanawake amesema kuwa ipo tabia ya
wanahabari hawa wa kike wachanga kujiendekeza ili wapate wepesi wa kufanya kazi bila kuwa wabunifu kujituma na
kuhakikisha wanajifunza kila mara ili kukomaa kitaaluma.
Pili Bi Mtambalike amesema kuwa
ipo haja ya kuwa na sera ya jinsia
katika vyombo vya Habari na kuhakikisha sera hizo zinatumika . Utafiti
uliofanywa katika vyombo 23 vya Habari sita tu ndio vilikuwa na sera
inayoeleweka ambayo haitumiki.
Hivyo tunaomba Jukwaa la Wahariri Tanzania –TEF liangalie
namna gani linaweza kuleta usawa wa kijinsia katika kuwa na idadi sawa ya wahariri kwa kuwa wanawake walio wengi wanaishia
katika ngazi ya Wahariri wasaidizi . Akitoa Takwimu amesema
asilimia 26 ya wanawake ndio wahariri
wasaidizi waliosalia wote ni jinsia ya
kiume wakiwemo wahariri wakuu wa jinsia ya kiume.
Pia, unyanyasaji huu wa
wanawake unafanyika hata kwenye upande wa vyanzo vya Habari ambavyo kwa
wanawake ni asilimia 36 ,a silimia
64 ya vyanzo vya Habari hutokana
na wanaume. Hivyo tunaomba hata wanawake
wanahabari walione hili na kuhakikisha wanawahoji wanawake wenzao kama chanzo
cha Habari badala ya kujikita zaidi kwa wanaume. Amesema Bi Mtambalike.
Naye Mhariri Mtendaji Bakatri
Machumu ambaye hakuweza kufika katika
hafla hiyo na kuwasilisha taarifa yake
kupitia video iliyorekodiwa amesema kuwa
kutokana na uzoefu wangu katika tasnia ya Habari waandishi wanawake ni wabunifu
na wananafasi kubwa ya kuangalia wanawake ambao wako katika jamii na
kusaidiana.
Naye Muwakilishi wa Umoja wa
Mataifa nchini Tanzania Bibi Hodan Addou
amesema “ Vyombo vya Habari ni kati ya vyombo vyenye nguvu kubwa hivyo vitumike
katika kuhakikisha vinaondoa kabisa suala zima la unyanyasaji na udhalilishaji
wa kijinsia katika vyomvo vya Habari”.
Pia, ameongeza kwa kusema kuwa
ni lazima kuhakikisha wanahabari wanawake wanashiriki kikamilifu katika kuhakikisha
wanatumia taaluma yao bila vikwazo ili kuwaletea maendeleo mtu momoj ammoja na Taifa kwa ujumla.
Akiongelea kauli mbiu ya mwaka
katika maadhimisho ya miaka miwili
ya Mtandao wa
Wanahabari Wananawake Tanzania na
Maafisa Uhusiano. Unaosema “Changamkia
Fursa sasa” Grabbing Opportunity now Katibu wa Kamati Mtandao wa
Wanahabari Wananawake Tanzania na
Maafisa Uhusiano, Bi Leah Mushi amesema
nafasi za mafunzo ambazo hutolewa na wadau mbalimbali wa sekta wa Habari
wakiwemo Wanawake wa Umoja wa Mataifa, pamoja na Shirika la Mitandao ya Habari-
Internews.
Aidha, kuna fursa nyingi za
mafunzo ya Mitandao ya kijamii na
pia wanatoa vitendea kazi kwa waandishi wachanga wake kwa waume ili waweze kujitegemea katika kufanya kazi zao na kujiendeleza
kitaaluma.
Naye Afisa Uhusiano wa Kituo cha
Umoja wa Mataifa nchini Tanzania Bi Stela Vuzo, amesema kuwa
huu ni wakati muafaka kwa wanahabari wachanga wanawake Tanzania
kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo
kwa ajili ya kusimamia taaluma ya Habari na
kujiendeleza, ikiwa ni pamoja na kupata kazi sehemu mbalimbali duniani na kuacha
kulalamika kuhusu masilahi na mishahara
midogo.
Haya tunayoyaona sasa inatokana na mfumo dume ambao tumeuishi
kwa miongo kadhaa ambayo adhari zake zinajitokeza , hivyo
sio kitu cha ajabu katika jamii
zetu, na hayatokei kwenye tasnia ya
Habari peke yake bali ni mfumo wa malezi
kwenye jamii zetu ambao unatakiwa ukemewa,
upigwe vita na uache kubagua
mtoto wa kike na yule wa kiume. Amesema
Mhariri Jesse Kwayu.
Iko haja ya Wadau wa Tasnia ya Habari
kuongeza kwa pamoja na kuona umuhimu wa sheria , kanuni na taratibu
tulizojiwekea ili kuifanya sekta ya Habari
iwe na mfumo madhubuti unaowafaidisha wana taaluma ya Habari kwa jumla.
No comments:
Post a Comment