Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein Ahudhuria Mahafali ya 15 ya SUZA d

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein asalimiana na Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako alipowasili katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA) Tunguu Wilaya ya Kati Unguja kuhudhuria hafla ya Mahafali ya 15 ya SUZA kulia Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar.Mhe. Riziki Pembe Juma na kushoto Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibare Dkt.Idrisa Muslim Hijja 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) Mhe.Dk.Ali Mohamed Shein akiwa katika Maandamano ya Mahafali ya 15 ya SUZA yaliofanyika katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein Tunguu Wilaya ya Kati Unguja kulia Makamo Mkuu wa SUZA Dkt. Zakia Mohamed Abubakar wakielekea katika ukumbi wa mahafari.
Mawaziri wa Elimu wa SMT na SMZ Prof.Joyce Ndalichako na Mhe.Riziki Pembe Juma wakiwa katika maandamano ya Mahafali ya 15 ya SUZA wakielekea katika ukumbi wa Dk. Ali Mohamed Shein SUZA Tunguu Wilaya ya Kati Unguja.



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.