Habari za Punde

Baadhi ya Vifaa vya Ujenzi wa Miundombinu ya Huduma za Maji Safi na salama pamoja na Ujenzi wa Majengo ya Huduma za Kijamii vilivyotolewa na Uongozi wa Jimbo la Aman katika Ukamilishaji wa Ilani ya Uchaguzi ndani ya Kipindi cha Miaka Minne.
Mbunge wa Jimbo la Amani Maalim Mussa Hassan akimuelezea Balozi Seif  hatua zilizochukuliwa na Uongozi wa Jimbo hilo katika Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
Mwakilishi wa Jimbo la Aman aliyevaa Kofia Mh. Rashid Ali Juma akimfahamisha Balozi Seif jitihada walizochukuwa za Ujenzi wa Tawi la Kwazee ikiwa ni Utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM.
Mwakilishi wa Jimbo la Aman Mh. RashidAli Juma akimuonyesha Balozi Seif baadhi ya Vifaa vya Ujenzi vinavyokamilisha Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi katika Kipindi cha Miaka Minne kuanzia Mwaka 2015.
Balozi Seif akimkabidhi Seti ya Jezi Mmoja Miongoni mwa Masheha waliomo ndani ya Jimbo la Amani kwa ajili ya Timu zao.
Balozi Seif akimkabidhi Vifaa vya Miundombinu ya Ujenzi Mmoja Miongoni mwa Masheha waliomo ndani ya Jimbo la Amani kwa ajili ya Shehia zao.
Balozi Seif akimkabidhi Saruji kwa ajili  ya Ujenzi wa Majengo ya Taasisi za Kijamii Mmoja Miongoni mwa Masheha waliomo ndani ya Jimbo la Amani kwa ajili ya Shehia zao.
Balozi Seif akimkabidhi Matofali na Saruji kwa ajili  ya Ujenzi wa Majengo ya Taasisi za Kijamii Mmoja Miongoni mwa Masheha waliomo ndani ya Jimbo la Amani kwa ajili ya Shehia zao.

Picha na – OMPR – ZNZ.




No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.