Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Mshauri,
Julius Ndyamukama (aliyesimama kulia) akitoa taarifa fupi kwa Waziri wa
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isaack Kamwelwe
(mbele), wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Ushauri ya TAA, (MAB) uliofanyika mwishoni
mwa wiki kwenye Jengo la TPA (One Stop Centre) jijini Dar es Salaam.
Na
Bahati Mollel,TAA
WAZIRI
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isaack Kamwelwe ameiasa Bodi ya
Ushauri ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (MAB), kutanguliza Utaifa na
Uzalendo mbele katika majukumu yao.
Kauli
hiyo ameitoa mwishoni mwa wiki katika halfa ya uzinduzi wa Bodi hiyo, ambao
umefanyika kwenye Jengo la Bandari nchini (TPA One Stop Centre) lililopo jijini
Dar es Salaam.
“Napenda
kutumia nafasi hii kuwaasa kwamba, nafasi hizi mlizopewa ni kwa ajili ya
kulitumikia Taifa letu kwa weledi, uaminifu na uadilifu mkubwa huku
mkitanguliza maslahi mapana ya taifa na uzalendo mbele”. Amesema Waziri
Kamwelwe
Pia
Waziri Kamwelwe ameitaka Bodi hiyo kuhakikisha inashirikiana bega kwa bega na menejimenti
ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), na taasisi za serikali hususan
Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) katika ujenzi wa viwanja vingi zaidi ya
wanavyovisimamia 58 kwa lengo ya kuviongeza, ili ndege za Shirika la ndege
Tanzania (ATCL) na mashirika mengine yaweze kupanua wigo wa safari.
Halikadhalika
amesema ulinzi na usalama katika viwanja vya ndege ukaimarishwe, ingawa bado
kunachangamoto ya kukosekana kwa uzio wa ndani na nje ya viwanja vya ndege,
ambapo pia suala la ugonjwa wa homa ya virusi vya Corona ulioanzia nchini China
lipewe kipaumbele kwa kuzingatiwa maslahi mapana ya Taifa yazingatiwe.
“Hili
la ugonjwa wa Corona liangaliwe kwa ukaribu zaidi ili viwanja vya ndege visiwe
ndio njia ya kuingiza ugonjwa huu, pia usalama wa watendajikazi uangaliwe pia,”
amesema na kuongeza.
“...
Vilevile mkahakikishe kuwepo na usimamizi mzuri wa wa ardhi na miundombinu ya
viwanja vyetu ikiwemo Jengo la Tatu la abiria –JNIA na utoaji wa huduma bora
zaidi kwa wateja, ukiangalia kwa sasa ni viwanja vichache tu ndio vina hati na
hili sio jambo jema, hakikisheni viwanja vyote vinapimwa na hati kupatikana,
kwani itasaidia kuongeza uhalali na kuongeza mapato ya TAA kwa kutumia ardhi
hiyo,” amesema Waziri Kamwelwe.
Pia
ameitaka Bodi hiyo kuhakikisha TAA inapata “control number” ili malipo mbalimbali
yatafanyika kupitia huko, ambapo pia ameitaka kubuni njia mbalimbali za
kuendesha viwanja vya ndege kibiashara, wakati sasa suala la TAA kuwa Mamlaka
zaidi badala ya sasa kuwa Wakala pamoja na kwamba lipo chini ya Wizara
linahitaji msukumo wa Bodi hiyo.
Hatahivyo,
Waziri Kamwelwe amesema pamoja na TAA kuwa na mafanikio bado inakabiliwa na
changamoto za kushindwa kuboresha miundombinu mbalimbali iliyopo viwanjani.
Bodi hiyo inaundwa na
Mwenyekiti Dkt. Masatu Chiguma na wajumbe ni Mhandisi Ven Kayamba, Dkt. Paschal
Mugabe, Mhandisi Daniel Kiunsi, Mhandisi Christopher Mukoma na Alex Haraba.
Awali
Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Mhandisi
Mshauri, Julius Ndyamukama amesema
Mamlaka hiyo imekuwa ikikua tangu kuanzishwa kwake hadi sasa, na kutolea mfano
wa mapato kuongezeka kutoka Shilingi Bilioni 6.3 hadi kufikia Bilioni 105.2 kwa
mwaka, ambalo ni sawa na ongezeko la asilimia 1,570.
Pia amesema Mamlaka
ilianza na ikiwa na miruko na mituo ya ndege 62,221 kwa mwaka na sasa imefikia
146,593 kwa mwaka ni sawa na ongezeko la asilimia 135.6.
Kwa upande wa abiria,
amesema ilianza ikiwa na idadi ya abiria 846,906 kwa mwaka na sasa imefikia
3,473,658 kwa mwaka ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 310.
Naye Mwenyekiti wa MAB,
Dkt. Masatu Chiguma, alimuahidi Waziri kuwa atafanya kazi bega kwa bega na TAA,
ili kufanikisha malengo yalilowekwa.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isaack Kamwelwe (wa nne kulia),
akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti Dkt Masatu Chiguma (wa nne
kushoto) na Wajumbe ya Bodi ya Ushauri ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
Tanzania (MAB), baada ya kuizindua Bodi hiyo mwishoni mwa wiki kwenye Jengo
la TPA.
Menejimenti
ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), leo wakiwa kwenye picha ya
pamoja na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isaack
Kamwelwe (mwenye suti ya maji ya bahari), na Mwenyekiti, Dkt Masatu Chiguma
na Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania
(MAB), iliyozinduliwa mwishoni mwa wiki kwenye Jengo la TPA.
No comments:
Post a Comment