KUFUATIA bidhaa kuwasili kisiwani Pemba zikitokea
Mkoani Tanga kwa ajili ya maandalizi ya Skukuu ya Eid, wananchi mbali mbali
wamekuwa wakijitokeza katika soko la Chake Chake kutafuta mahitaji hayo.
BIASHARA ya Viungo mbali mbali vya vyakula huwa
maarufu katika kipindi cha kuelekea Skukuu, pichani kijana akiuza viungo hivyo
kama alivyokutwa na mpiga Picha.
WANANCHI wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kuwatafutia
watoto wao mahitaji ya skukuu kama suruali, pichani baadhi yao wakinunua nguo
kuelekea maandalizi ya skukuu.
BIASHARA ya Viungo mbali mbali vya vyakula huwa
maarufu katika kipindi cha kuelekea Skukuu, pichani kijana akiuza viungo hivyo
kama alivyokutwa na mpiga Picha.
BIASHARA ya Viatu vya Kimasai vimekua vikipendwa na
wananchi wengi kwa ajili ya kuvalia kanzu wakati wa kwenda msikini, hususan
katika kipindi cha kuelekea skukuu inapowadia, pichani wananchi wakichagua
viatu hivyo katika eneo la machomanne.
IKIWA Mwezi Mtukufu wa Ramadhani unaelelekea
Ukingoni, biashara ya mikungu na vyungu huwa maradufu katika mji wa chake
chake, pichani muuza mikungu, vyungu na viotezo akipanga biashara yake.
BAADHI ya Akina mama wakiawachagulia watoto wao nguo
za kiume katika maeneo ya mji wa Chake Chake, ikiwa ni kuelekea skukuu ya Eid.
WANANCHI mbali mbali wakiwatafutia watoto wao wa
kike nguo za skukuu, katika maeneo ya mji wa Chake Chake ikiwa ni baada ya
kumalizika kwa mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
MAANDALIZI ya skukuu tayari yameanza biashara ya
samli na siagi nayo imekua kwa wingi katika kipindi cha kuelekea skukuu,
pichani mmoja ya wafanya biashara wa samli akipima samli hiyo.
BIASHARA ya mayai nayo haiku nyuma katika maandalizi
ya skukuu, ambapo treya moja inauzwa shilingi 12000 hadi 1100, katika maeneo ya
Chake Chake.
BAADHI ya wauzaji wakuku wa Kiswahili wakiwa
wametulia katika soko la Kuku Chke Chake, wakisubiri wateja wa biashara hiyo
kuelekea skukuu ya Eid.
(Picha na Abdi Suleiman - Pemba)
No comments:
Post a Comment