Habari za Punde

Viongozi Rukwa waendelea kuhamasisha matumizi ya Nyungu

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo, akisisitiza jambo wakati wa hafla ya mkutano wa Baraza la Madiwani 
  Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda  akzungumza wakati wa Kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri 
Baadhi yaWataalamu waliohudhuria kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri kilichohusu utekelezaji wa hoja za ukaguzi na mapendekezo ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali nchini.
Baadhi ya Madiwani waliohudhuria kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri kilichohusu utekelezaji wa hoja za ukaguzi na mapendekezo ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali nchini.

Na.Abdul rahman Salim
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa wito kwa wananchi na wadau wote mkoani humo kuhakikisha wananchukua hatua za tahadhari ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona (Covid-19) kwa kufuata maelekezo ya wataalamu wa Afya pamoja na kushauri matumizi ya Nyungu kwaajili ya kujifukiza.

Amehamasisha hayo ikiwa ni katika kuunga mkono kauli ya Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) pamoja na viongozi wengine wa juu nchini katika kupambana na Covid – 19 ambao huenezwa kwa kuingiwa na majimaji yatokayo kwa njia ya hewa wakati mgonjwa anapokohoa au kupiga chafya au kugusa majimaji yanayotoka puani mwa mtu aliyeathirika.

“Nitoe wito kwa wadau wote ikiwa ni pamoja na nyini waheshimiwa madiwani kuchukua hatua za tahadhari ya ugonjwa huu kwa kufuata maelekezo ya wataalamu wetu wa afya. Tukumbuke kuwa virusi vya Corona ni janga la kidunia na linaua, Aidha matumizi ya Nyungu kwaajili ya kujifukizia yanashauriwa na Mh. Jafo waziri wa OR-TAMISEMI pamoja na viongozi wengine wa juu tuyazingatie, watu wapige Nyungu,” Alisisitiza.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Nkasi ambaye pia anakaimu Wilaya ya Sumbawanga Mh. Said Mtanda akifafanua michanganyiko ya aina tatu inayoshauriwa na wataalamu wa tiba ya asili yaliyofanyiwa majaribio na kituo cha Tiba asili kinachotambulika na serikali amesema moja ya mchanganyiko ni kutumia mti wa mwarobaini, tangawizi iliyopondwa, majani ya mpera, limao zilizokatwa  unachemsha pamoja na kisha kujifunika na kuvuta moshi kwa pua na mdomo ili moshi huo uingie mwilini na hatimae kwenda kuua virusi vya Corona.

“Sisi kule Namanyere (Wilayani Nkasi) tumeweka utaratibu wa kuhamasishana kujifukiza, kwasababu ukiona aibu matatizo kweli utayapata, kwahiyo kiongozi ukiwa unajifukiza unakapiga kapicha kidogo unawatumia wengine ili waseme hee hata Diwani kajifukiza, kwahiyo wale unaowaongoza watahamasiska kujifukiza kwasababu wataona kumbe sasa hili sio suala la aibu,” Alisema.

Viongozi hao wamesema hayo wakati wa vikao vya madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo na Wilaya ya Sumbawanga katika vikao vya Mabaraza ya Madiwani ya Halmashauri hizo kuhusu utekelezaji wa hoja za ukaguzi na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali nchini. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.