Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein Amuapisha Mkuu wa Wilaya Mpya na Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Mipango.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Dk.Juma Malik Akil kuwa Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Zanzibar katika hafla iliyofanyika leo Ikulu Mjini Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Mkuu mpya wa Wilaya ya Wete Pemba Kamanda Mohamed Mussa Seif  (Mkobani). katika hafla iliyofanyika leo Ikulu Mjini Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni akiwemo  Kamanda Mohamed Mussa Seif (Mkobani) kuwa Mkuu mpya wa Wilaya ya Wete

Rais Dk. Shein amemuapisha Mkuu huyo mpya wa Wilaya ya Wete kufuatia uteuzi wake alioufanya hivi karibuni baada ya kutengua uteuzi wa aliyekwua Mmkuu wa Wilaya hiyo ya Wete, Kapteni Khatib Khamis Mwadini.

Kabla ya uteuzi huo Kamanda Mohamed Mussa Seif (Mkobani) alikuwa Mkuu wa Kamandi ya KMKM Pemba.

Mwengine alieapishwa hivi leo katika hafla hiyo ni Dk. Juma Malik Akil ambaye anakuwa Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Zanzibar.

Hafla ya kuwapishwa viongozi hao  ilifanyika Ikulu Jijini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar akiwemo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu pamoja na Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Wengine ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali Said Hassan Said, Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee pamoja na Makatibu Wakuu wengine.  

Aidha, hafla hiyo pia ilihudhuriwa na Mkuu wa  Mkoa wa Mjini Magharibi Hassan Khatib Hassan, Viongozi wa Vikosi vya SMZ, Washauri wa Rais wa Zanzibar, viongozi wengine wa Serikali pamoja na wanafamilia.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.