Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Ali Mohamed Shein Atowa Mkono wa Polev Kwa Famiulia ya Marehemu Haji Nassib Haji Nyanya


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiitikia dua ya kumuombea Marehemu Mzee Haji Nassib Haji Nyanya na (kushoto kwa Rais) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein na Wanafamilia wakiitikia dua, alipofika kutowa mkono wa pole kwa Familia ya marehemu nyumbani kwake Bububu kwa Nyanya

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, ametoa mkono wa pole kwa familia ya Marehemu Mzee Haji Nasibu Haji Nyanya aliyefariki dunia alfajiri ya kuamkia Jumamosi ya Julai 11, 2020 huko Jijini Dodoma.
Rais Dk. Shein alifika nyumbani kwa marehemu haji Nasibu Nyanya mara tu baada ya kurejea Jijini Dodoma ambako alishiriki katika vikao mbali mbali vya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Akiwa nyumbani kwa Marehemu Haji Nasibu Haji Nyanya huko Bububu, Rais Dk. Shein aliwapa mkono wa pole wanafamilia wote akiwemo mjane wa Marehemu Bi Zainab Nyanya na kuwataka kuwa na subira katika kipindi hichi kigumu cha msiba.
Rais Dk. Shein akiwa amefuatana na Mama Mwanamwema Shein aliitaka familia hiyo kumuombea dua Marehemu Haji Nasibu Haji Nyanya ambaye alikuwa ni mwanasiasa mkongwe na mfanyabiashara wa muda mrefu.
Katika salamu zake hizo za pole, Rais Dk. Shein alieleza jinsi alivyoguswa na kifo cha Mzee Nyanya ambacho kilitokea huko Jijini Dodoma na kueleza jinsi walivyokuwa pamoja na Marehemu kabla ya kumfika umauti.
Nayo familia ya Mzee Nyanya ilitoa shukurani kwa Rais Dk. Shein kwa kushirikiana nao bega kwa bega katika msiba huo yeye pamoja na Mama Shein ikiwa ni pamoja na kwenda kuwapa mkono wa pole mara tu baada ya kurudi safari.
Marehemu Mzee Nyanya atakumbukwa katika harakati mbali mbali za kisiasa, kiuchumi na kijamii hapa nchini ambapo mnamo  Januari 8 mwaka huu 2020 Rais Dk. Shein alimtunuku Nishani ya Mapinduzi kwa Viongozi na Wananchi Wenye Sifa Maalum huko katika viwanja vya Ikulu Jijini Zanzibar.
Marehemu ameacha mjane, mtoto mmoja na wajukuu wanne, MwenyeziMungu ailaze roho yake mahala pema peponi, Amin.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.