Na Jaala Makame Haji-- ZEC
Tume
ya Uchaguzi ya Zanzibar ZEC itagawa vitambulisho vya Kupigia Kura tarehe 25 na
26/7/2020 kwa Wilaya zote za Unguja baada ya kukamilika ugawaji huo katika
Wilaya za Pemba wiki iliyopita.
Mkurugenzi
wa Uchaguzi ZEC THABIT IDAROUS FAINA wakati akizungumza na watendaji ambao
wameteuliwa kusimamia kazi hiyo katika vituo vya Unguja alisema, Tume imeandaa
utaratibu maalum ambao utarahisha zoezi hilo kufanyika kwa urahisi zaidi.
Mkurugenzi
Faina, aliwataka watendaji walioteuliwa kutoa elimu kwa wapiga kura ya kutumia
huduma ya mtandao wa Zantel ambayo itawawezesha Wapiga Kura wanaokwenda
kuchukua vitambulisho vyao kupata huduma hiyo kwa haraka Zaidi na bila ya
usumbufu wa aina yeyote.
“Kwa
kutumia mtandao wa Zantel unaweza kupiga *152*29# ili kujua kibox ambacho kipo
kitambulisho chako cha kupigia kura”
Ndugu
Faina alisisitiza kuwa, malengo ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ni kuendesha
Uchaguzi mkuu ambao utazingatia misingi ya haki, uhuru na uwazi
Mkuu
wa kurugenzi ya Elimu ya Wapiga Kura, Habari na Mawasiliano kwa Umma Tume ya
Uchaguzi ya Zanzibar JUMA SANIFU SHEHA aliwataka watendaji hao huifanya kazi
hiyo kwa uadilifu, uaminifu na umakini wa hali ya juu ili kusaidia kuondosha
malalamiko baina yao.
Naye
Msimamizi wa Uchaguzi Wilaya ya Mjini SAFIA IDDI MUHAMMAD na Msimamizi wa
Uchaguzi Wilaya ya Magharibi “B” FATMA GHARIB HAJI, kwa wakati tofauti waliasa watendaji
kutumia lugha nzuri wakati wanapokuwa vituoni kutoa huduma pamoja na kuzingatia
sera ya jinsia na ushirikishwa wa makundi ya kijamii ya mwaka 2014
iliyoanzishwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ambayo inawaelekeza Tume kuwapata
fursa watu wenye mahitaji maalum.
Watendaji
walioteulia kusimamia ugawaji wa Vitambulisho katika Vituo vilivyotumika
kuandikisha Wapiga kura kwa kazi ya uandikishaji iliyopita wamepongeza
utaratibu uliowekwa na Tume katika kutoa huduma vituoni ambayo itawapa urahisi wa kufanya kazi hiyo.
Mafunzo
hayo yametolewa kwa watendaji wote wa Wilaya za Unguja walioteuliwa kusimamia
kazi ya ugawaji wa vitambulisho vya Wapiga Kura.
No comments:
Post a Comment