Habari za Punde

Benki ya NMB yanogesha Siku ya Kizimkazi Zanzibar! na Kukabidhi Jengo la Vyoo lenye Matundu 10 Kwa Skuli ya Msingi Kibuteni Wilaya ya Kusini Unguja.

Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi kutoka kwa Meneja wa NMB kanda ya Dar es Salaam-Donatus Richard alipotembelea akina mama wajasiriamali wanaodhaminiwa na Benki hiyo kwenye  hafla ya Kizimkazi Day  Wilaya ya Zanzibar. Akishuhudia ni Meneja Masuala ya Uwajibikaji kwa Jamii – Bi Lilian Kisamba (mwenye koti)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Meneja wa Banki ya NMB kanda ya Dar es salaam na Zanzibar  Donatus Richard alipotembelea maonesho ya siku ya Wakizimkazi yanayofanyika kila Mwaka katika kijiji cha Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja leo Agosi 13,2020. kulia Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahamoud  .

Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizungumza na Maafisa wa Benki ya NMB katika hafla ya kukabidhi  msaada wa vyoo vya matundu 10 vyenye thamani ya sh. Milioni 10/- kwa shule ya Msingi Kibuteni  iliyopo Zanzibar Wilaya ya Kusini Unguja 
Jengo la choo cha matundu 10 lililokabidhiwa na Benki ya NMB kwa matumizi ya wanafunzi wa  shule ya Msingi Kibuteni Zanzibar Wilaya ya Kusini.


Benki ya NMB inaendelea kuboresha miundombinu na mazingira ya shule  visiwani Zanzibar kwa kutoa vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya shilingi Milioni 10/- zilizofanikisha ujenzi wa vyoo vyenye matundu 10 katika shule ya Kibuteni iliyopo Wilaya ya Kusini. NMB pia imetoa tisheti 300- ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono sherehe za Kizimkazi ‘Kizimkazi Day’ zinazofanyika kila mwaka mwezi wa nane - Lengo ikiwa ni kutathmini shughuli za kimaendeleo katika maeneo ya Kizimkazi na kuangali changamoto zilizopo ili kuzipatia utatuzi.

Siku hii huratibiwa na Makamu wa Rais- Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na viongozi wengine wa Serikali visiwani humo. Akizungumza katika hafla ya makabidhiano, Mheshimiwa Samia ameishukuru Benki ya NMB kwa namna inavyokuwa mstari wa mbele kuchangia huduma za kijamii mbalimbali kama Elimu, Afya na Maafa. Ni miaka mingi sasa, Benki ya NMB imekua ikitoa asilimia 1℅ ya faida yake kama sehemu ya uwajibikaji kwa jamii inayowanzunguka.


Akizungumza Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam - Donatus Richard ameeleza kuwa, utoaji wa elimu kwa vijana ni suala la kipaumbele sana na kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu NMB imekuwa ikiwawezesha vijana kupata elimu ya fedha na kujifunza kuweka akiba katika umri mdogo kupitia program yake ya WAJIBU -Jifunze, Jipange Wajibika’ –  katika shule za msingi na secondary Tanzania. ikilenga vijana kujifunza umuhimu wa kuweka akiba na mipango kwaajili ya maendeleo yao na kukidhi mahitaji muhimu ya baadae. Kupitia program hii wameweza kuwafika zaidi ya vijana 70,000 nchini.

NMB inatambua kwamba ili mtu aweze kuimarika kifedha, ni lazima ajenge mtazamo unaofaa kuhusu matumizi ya fedha. Hivyo basi, wamekuwa wakiwaelimisha Wajasiriamali Wadogo na wa Kati; Kupitia Klabu za Biashara za NMB, wajasiriamali wa kati na wadogo wamekuwa wakipewa elimu juu ya masuala yanayohusu mipangilio ya biashara, utunzaji wa vitabu vya fedha, mipangilio ya fedha, kukopa na elimu katika maeneo mengine ya fedha kama yalivyoombwa na wanachama. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.