Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Ali Mohamed Shein na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Balozi Seif Ali Iddi, wakiitikia dua ikisomwa na Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh. Hassan Othman Ngwali (kushoto kwa Rais) baada ya kumaliza kisoma cha hitma kumuombea marehemu iliofanyika katika Msiki wa Upenja Mkoa wa Kaskazini Unguja leo.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj
Dk. Ali Mohamed Shein leo ameongoza
mazishi ya Mweyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Amani Kichama marehemu
Juma Khamis Haji (Juma Resi), yaliyofanyika kijijini kwao Upenja, Wilaya ya Kaskazini ‘B’, Mkoa wa Kaskazini
Unguja.
Viongozi mbali mbali
wa vyama vya siasa na serikali, pamoja na wananchi, ndugu na jamaa walihudhuria
katika mazishi hayo akiwemo Makamo wa
Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, Naibu Katibu wa CCM Zanzibar
Abdallah Juma Mabodi pamoja na Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman
Ngwali.
Mapema Alhaj Dk. Shein
aliungana na viongozi, ndugu, jamaa, marafiki na wananchi mbali mbali katika
sala ya kumsalia Marehemu Juma Resi katika
Msikiti wa Upenja, Wilaya ya Kaskazinii ‘B’, Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Katika uhai wake
Marehemu Juma Khamis Haji (Juma Resi), aliyezaliwa mwaka 1951 amekitumikia
Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika nyadhifa mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuwa Diwani
wa Jimbo la Muembemakumbi, Katibu wa Jimbo la Muwembemakubi, Mwalimu wa
Madarasa ya Itikadi pamoja na makundi ya Vijana wa Hamasa.
Nafasi nyengine ni
Afisa Uhamasishaji Wilaya, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa na Mjumbe wa
Mkutano Mkuu wa Mkoa, Katibu Mwenezi Wilaya ya Mjini, Katibu Mwenezi Wilaya ya
Amani, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya
Amani Kichama, cheo ambacho alikitumikia mpaka mauti yalipomfika.
Wakati huo huo, mara
baada ya mazishi, Alhaj Dk. Shein alikutana na familia ya marehemu Juma Resi
hapo hapo kijijini kwao Upenja na kutoa mkono wa pole kwa familia na wafiwa
wote pamoja na kumuomba Mwenyezi Mungu awape subira katika kipindi hiki kigumu
cha msiba huku akisisitiza kuendelea kumuombea dua marehemu.
Marehemu Juja Resi ameacha
vizuka wawili pamoja na watoto kumi na mbili (12) na Wajukuu 23, Mwenyezi Mungu
ailaze roho ya maremu mahala pema peponi, Amin.
Rajab
Mkasaba, Ikulu
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment