Waziri wa Mawasiliano naTeknolojia ya Habari, Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (wa tatu kulia) akishuhudia Makabidhiano ya mkataba ya kazi ya ujenzi, uwekaji na usimikaji wa majina ya mitaa/ barabara na namba za nyumba katika halmashauri 12 nchini, baina ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula (wa tatu kushoto) na mwakilishi wa kandarasi ya Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT) katika hafla iliyofanyika viwanja vya Bunge, jijini Dodoma. Kulia Naibu Waziri Mhe. Mhandisi Kundo Mathew na Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt Jim Yonazi.
Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt Zainab Chaula akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa kandarasi ya Raddy Fibre Solution Ltd, Ramadhani Hassani Mlanzi mkataba wa kazi ya ujenzi wa Miundombinu ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano katika hafla iliyofanyika katika viwanja vya Bunge, jijini Dodoma. Kulia ni Waziri wa Wizara hio Mhe.Dkt. Faustine Ndugulile na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Jim Yonazi wakishuhudia.
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Kulia) akizungumza na wakandarasi, Menejimenti ya Wizara hiyo na waandishi wa habari katika hafla ya makabidhiano ya mikataba ya kazi ya ujenzi wa Miundombinu ya Mawasiliano baina ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula (katikati) na wakandarasi hao katika viwanja vya Bunge, jijini Dodoma. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt Jim Yonazi.
Na Faraja Mpina- WMTH
Waziri
wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile amewaagiza wakandarasi wanaokwenda kutekeleza miradi minne ya miundombinu ya mawasiliano yenye thamani ya
shilingi bilioni 7.5,
kuhakikisha wanafanyakazi usiku na mchana ili kukamilisha kazi hiyo ndani ya muda wa mkataba bila kuongeza hata siku moja ya ziada.
Dkt.
Ndugulile alizungumza hayo alipokuwa katika hafla ya makabidhiano ya mikataba ya kazi hiyo baina ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt.
Zainab Chaula na wakandarasi hao wazalendo ambao ni Shirika la Mawasiliano Tanzania
(TTCL), Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) na Raddy Fibre Solution Ltd katika viwanja vya
Bunge, jijini Dodoma.
Miradi hiyo ni pamoja na kujenga,
kupanua na kuunganisha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ili kuunganisha na kuimarisha mawasiliano kutoka Mkoa wa Singida hadi Mkoa wa Mbeya,
maeneo ya Mkoa wa Mtwara ili kuunganisha mawasiliano kati ya Tanzania
na Msumbiji na kutoka eneo la Mji wa Serikali Mtumba hadi Msalato jijini Dodoma.
Aliongeza kuwa jumla ya kilo mita
409 zitaunganishwa na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano katika maeneo hayo na Halmashauri 12
nchini zitawekewa vibao vya majina ya mitaa/barabara na namba za nyumba katika kutekeleza Mradi wa anwani
za makazi na posti kodi.
Dkt.
Ndugulile amesema kuwa lengo ni kuhakikisha mpaka kufikia mwaka 2025 asilimia 80 ya wananchi wanapata mawasiliano ya uhakika na kushiriki katika kuinua uchumi wa kidijitali kupitia biashara mtandao,
ambapo mnunuzi na muuzaji lazima wawe na mawasiliano ya mtandao na mnunuzi kuwa na anwani ya makazi ili afikishiwe bidhaa aliyonunua mpaka nyumbani kwake.
“Sina shakana wakandarasi wazalendo,
mtajiengua ni nyinyi wenyewe iwapo mtakuja na visingizio vya kutokamilisha kazi kwa wakati,
mkafanye kazi mchana na usiku kuhakikisha miradi inakamilika ndani ya muda wa mkataba na ubora unaokubalika”,
Dkt. Ndugulile
Aidha
Dkt. Ndugulile amesema kuwa Wizara inaendelea na mchakato wa kushughuliki asuala la
vifurushi na bando na kuomba wananchi kuwa na subira mpaka mwisho wa mwezi huu ili Wizara kuja na tamko rasmin ambalo halitaathiri mapato ya watoa huduma, mapato ya Serikali na vile vile kutomuathiri mwananchi.
Katika hatua nyingine,
Dkt. Ndugulile ametoa rai
kwa wananchi wasipokee maelekezo yeyote kuhusu miamala binafsi kwa njia ya simu bali njia sahihini kwenda kwenye vituo vya mawakala vinavyotambulika na vilivyosajiliwa na makampuni ya simu.
“Tunataka kuimarisha mifumo ya mawakala wa makampuni ya simu ili kuweza kuwabaini na kuwachukulia hatua mawakala ambao sio waaminifu”,
Dkt. Ndugulile
Amesema kuwa,
Serikali imeanza mkakati wa kushughulika na watu wanaotoa lugha za matusi, kashfa na utapeli mitandaoni ambapo mpaka sasa genge la watu 17
wanaoongoza genge la uhalifu mitandaoni waliokuwa wamejificha mkoani Morogoro
wameshakamatwa na muda wowote watapandishwa mahakamani.
Ameongeza kuwa Serikali inania njema ya kujenga mazingira wezeshi ya kuweza kutumia mitandao ya mawasiliano na katiba ya nchi inaruhusu wananchi kukosoa kwa lugha ya staha, huku akisisitiza kuwa lugha
za matusi, kashfa na kejeli hazitovumilika.
Imetolewa na Kitengo
cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.
No comments:
Post a Comment