Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akizungumza na Afisa Mtendaji Mkuu wa Anglogold Ashanti – Afrika, Bw. Sicelo Ntuli wakati walipokutana kwa mazungumzo leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiongoza
kikao chake na Kampuni ya Madini ya Anglogold Ashanti ya Afrika Kusini kilichofanyika
leo jijini Dar es Salaam
Na Mwandishi wetu, Dar
Kampuni ya Madini ya
Anglogold Ashanti ya Afrika Kusini imeahidi kuendeleza ushirikiano na Serikali
ya Tanzania katika sekta ya madini na kuhakikisha kuwa sekta hiyo inakuwa
mstari wa mbele kuchangia uchumi.
Ahadi hiyo imetolewa na
Afisa Mtendaji Mkuu wa Anglogold Ashanti – Afrika, Bw. Sicelo Ntuli wakati
alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) leo Jijini Dar es Salaam.
Akiongea mara baada ya
mazungumzo hayo Balozi Mulamula amesema kuwa, Anglogold Ashanti ni wadau
wakubwa katika sekta ya madini na wameonesha utayari wao wa kushirikiana kwa
karibu na Serikali katika kukuza na kuendeleza sekta ya madini.
“Leo hii nimekutana na
uongozi wa Kampuni ya Madini ya Angogold Ashanti na tumejadili pamoja na mambo
mengine, utayari wa Kampuni hiyo kushirikiana na Serikali katika kukuza sekta
ya madini hapa nchini,” Amesema Balozi Mulamula
Balozi Mulamula ameongeza
kuwa kitendo cha kukutana na wadau wa madini kama Anglogold Ashanti na
kujadiliana nao masuala mbalimbali ya ushirikiano wa kukuza sekta ya madini ni
sehemu ya utekelezaji wa sera ya Diplomasia ya Uchumi.
Kwa Upande wake, Afisa
Mtendaji Mkuu wa Anglogold Ashanti Bw. Ntuli amesema kuwa uongozi wa Anglogold
umefarijika kukutana na Mhe. Waziri wa Mambo ya Nje na kuweza kujadiliana nae
mambo mbalimbali ikiwemo suala la kukuza ushirikiano baina ya Kampuni hiyo na
Serikali ya Tanzania.
“Sisi kama Anglogold
tumefarijika kuona Serikali ya Tanzania ipo tayari kuendeleza ushirikiano na
Sisi…….tunaahidi kuendeleza ushirikiano huu kwa maslahi mapana ya pande zote
mbili,” Amesema Bw. Ntuli
Aprili 16, 2021 Kampuni ya Anglogold Ashanti iliingia ubia na Kampuni ya BG Umoja ya nchini Tanzania kwa ajili ya kuchimba madini katika miradi ya Nyankanga na Geita Hill. Anglogold ni Kampuni mama ya Geita Gold Mine (GGML) imeipatia BG Umoja mkataba wenye thamani ya Dola za Marekani Milioni 186 kwa miaka miwili.
No comments:
Post a Comment