Habari za Punde

Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje na Ulinzi na Usalama Yatembelea Mradi wa Nyumba za Polisi Kunduchi,Mikocheni na Oysterbay Jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Khamis Hamza Chilo (wapili kushoto) akiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama, Mussa Zungu(wakwanza kulia) na Inspekta Jenerali wa Polisi nchini, Simon Sirro(wapili kulia), wakitoka ndani ya Kituo cha Polisi Oysterbay ikiwa ni ukaguzi wa Mradi uliohusisha kituo hicho, nyumba za polisi zilizopo Mikocheni na Kunduchi.Ziara hiyo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama, Mussa Zungu akiongoza msafara wa kukagua Mradi wa Nyumba za Polisi Mikocheni(zinazoonekana pichani) ambapo mradi huo unahusisha Kituo cha Polisi Oysterbay,Nyumba za Makazi ya Askari zilizopo Kunduchi na Mikocheni.Ziara hiyo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama, Mussa Zungu akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Khamis Hamza Chilo (katikati),wakati wa ziara ya Ukaguzi wa Mradi  unaohusisha Kituo cha Polisi Oysterbay,Nyumba za Makazi ya Askari zilizopo Kunduchi na Mikocheni.
Kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini,Simon Sirro na wengine ni wajumbe wa kamati hiyo na watumishi wa wizara.Ziara hiyo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.