Habari za Punde

Katibu wa Itikadi na Unezi CCM Taifa Ndg. Shaka Atoa Asante Kwa Wananchi wa Konde Kwa Kuendelea Kuimamini CCM.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM Itikadi na Uenezi Ndg,Shaka Hamdu Shaka akizungumza na Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali (hawapo pichani) wakati akitowa shukrani kwa Wananchi wa Jimbo la Konde Pemba, kwa kuipatia ushindi CCM katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo hilo. 

Na Bashir Nkoromo, CCM Blog

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimewashu Wananchi wa  Jimbo la Konde katika Wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba kwa kuendelea kukiamini na kukipatia ushindi wa kishindo katika  uchaguzi mdogo wa jimbo la hilo.


Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka amesema kutokana na imani hiyo ya Wananchi,  katika Uchaguzi huo mgombea wa CCM Sheha Mpemba Faki ameweza kushinda  kwa kura 1796 ambazo ni za kishindo.


Jimbo hilo lilikuwa chini ya upinzani kwa miaka 15 na kwamba Konde ni Jimbo la tatu CCM kushinda tangu  Rais Samia Suluhu Hassan achaguliwe kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi.


Shaka amesema, mbali ya kushinda Ubunge jimbo la Konde, CCM imepata ushindi katika Kata 6 katika Uchaguzi mdogo wa Udiwani Tanzania Bara na kuzitaja Kata hizo kuwa ni Mbagala Kuu iliyopo Manispaa ya Temeke mkoani Dar es Salaam na Kata ya Ndirigishi iliyopo Kiteto mkoa wa Manyara.


Kata zingine ni Mitesa iliyopo Wilaya ya Masasi mkoa wa Mtwara, Gare iliyopo Wilaya ya Lushoto mkoa wa Tanga, Mchemo iliyopo Wilaya ya Newala mkoa wa Mtwara na Kata ya Chona iliyopo Wilaya ya Ushetu mkoa wa Shinyanga. 


"Ushindi huu umetokana na uaminifu na uadilifu wa Chama Cha Mapinduzi katika kuwasikiliza na kuwatumikia wananchi, aidha  unatuongezea ujasiri na nguvu zaidi katika kuendelea kuwatumikia watanzania. 


CCM inaahidi  kuendelea kuwatumikia kwa usikivu, bidii kubwa amani na utulivu kwa kuwa tunao uzoefu mkubwa wa kufanya hivyo", amesema Shaka na kuongeza;


"Chaguzi hizi zinaendelea kutoa funzo kwa vyama vya Upinzani nchini kuwa wasiendelee kutafuta  mchawi bali wakae chini wajitafakari na wajadili mtazamo wa namna wanavyofanya na kuendesha siasa zao, sivyo kama wataendelea kutegemea siasa za ukosoaji wa makosa ya serikali inayongozwa na CCM kwa kutumia hoja ambazo hazijafanyiwa utafiti wa kutosha basi utawaoandosha katika ramani za siasa nchini".

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.