Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi Amejumuika Katika Sala ya Ijumaa na Katika Sala ya Kuusalia Mwili wa Marehemu Mke wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchumi wa Buluu Dkt. Aboud Suleiman Jumbe Masjid Mushawar Muembeshauri Jijini Zanzibar.alia Mwin

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Viongozi wa Serikali na Dini baada ya kuwasili katika Viwanja vya Masjid Mushawar Muembeshauri Jijini Zanzibar, kuhudhuria Ibada ya Sala Ijumaa iliofanyika katika Masjid hiyo. 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (wa tatu kulia) akishiriki katika Sala ya Maiti ya Marehemu  Mke wa Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Dk.Aboud Suleiman Jumbe katika Masjid Mushawal Mwembe shauri Jijini Zanzibar baada ya Sala ya Ijumaa na maziko kufanyika leo katika makaburi ya Mwanakwerekwe Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi (wa pili kulia) pamoja na waumini mbali mbali na wananchi wakiitikia Dua iliyoombwa na Mufti Mkuu wa zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi (wa tatu kulia) baada ya  Sala ya Maiti ya Marehemu Mke wa Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Dk.Aboud Suleiman Jumbe katika Masjid Mushawal Mwembeshauri Jijini Zanzibar baada ya Sala ya Ijumaa na maziko kufanyika leo katika makaburi ya Mwanakwerekwe Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, leo amejumuika na mamia ya waumini wa Dini ya Kiislamu katika Ibada ya sala ya Ijumaa, iliofanyika Masjid Mushawar, Mwembeshauri Jijini Zanzibar.

Akisoma khutuba ya sala hiyo, Sheikh Mziwanda Ngwali Ahmad amewataka binaadamu kutokusahau neema kubwa waliyozuruzukiwa na Mwenyezi Mungu na kubainisha udhaifu walionao mbele ya Muumba.

Amesema binadamu wanapaswa kutambuwa  udhaifu wao unaotokana na maumbile waliyonayo.

Sheikh Mziwanda aliwataka waislamu kumuogopa Mwenyezi Mungu na kudumu katika kufanya mambo mema kwa kutambua utukufu alionao mola wao.

Alisema pamoja na udhaifu walionao binadamu, Mwenyezi Mungu amewatukuza  binaadamu na hivyo akatumia fursa hiyo kumuomba Mwenyezi Mungu kuwapa malipo mema waja wake.

Aidha, aliwataka waislamu kuondokana na jeuri na kiburi kwa ajili ya asili zao, nasaba, mali au elimu waliyonayo.

Wakati huo huo, Rais Dk. Mwinyi  alishiriki katika sala ya kumuombea dua maiti ya mke wa  Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Aboud Suleiman Jumbe, ambae amezikwa mchana huo katika makaburi ya Mwanakwerekwe  Unguja.

Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822 

 E-mail: abdya062@gmail.com.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.