Na Raya Hamad – OMKR
Watendaji
na wafanyakazi wa Tume ya Kitaifa Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya
wametakiwa kudumisha nidhamu katika maeneo yao ya kazi na kuhakikisha
wanatimiza majukumu yao kwa ufanisi
Katibu
Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Dkt Omar D. Shajak ameyasema hayo kwenye
kikao cha watendaji na wafanyakazi wa Tume hio ikiwa ni mfululizo wa ziara zake
katika kutembelea taasisi zinazosimamiwa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais
Amewakumbusha
watendaji na wafanyakazi hao kusimamia vyema majukumu yao kama yalivyoelekezwa
kwenye mpango wa majukumu ya kazi waliopewa na kuacha kufanya kazi kwa mazoea
ikiwemo uingiaji kazini na utokaji wa kazini
Dkt
Shajak amesema mapambano ya Dawa za kulevya yanaanzia ofisini hivyo wanawajibu
wa kutunza siri, kuwa waadilifu, watiifu na wazalendo katika kuitumikia
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ambayo imewaamini na kuwaweka walipo
Amesema
mapambano ya dawa za kulevya hayatakwisha iwapo hakutakuwa na mashirikiano
yanayoanzia ndani ya taasisi yenyewe hivyo ni wajibu wa kila mmoja kuchukuwa
tahadhari katika mapambano haya kwani ni vita ya wenye fedha wanaongalia
maslahi yao pekee
“isije
kufika mahali ukajiona wewe ndio mtoa habari za ndani hatutamuonea mtu muhali
na iwapo mtu anaona hawezi kutunza siri haendani na sheria na taratibu za Tume
hii ambayo inaelekea kuwa Mamlaka kamili basi mapema ajisalimishe milango iko
wazi mapambano ya dawa za kulevya ni yetu sote hakuna aliyekuwa hajaguswa
kuanzia mtumiaji mwenyewe, si wazazi, walezi , familia na hata majirani wote
tunaathirika wizi umekithiri na mambo mengine yasiyo na maadili”
Katibu
Dkt amewaahidi wafanyakazi hao kuwa Serikali inatambua changamoto zao na zinafanyiwa
kazi kwa hatua ikiwemo ufinyu wa ofisi na uhaba wa wafanyakazi kwani ni masuala
ya kiutawala
Mkurugenzi
Mkuu Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya Kanal Burhani
Z. Nassor amesema Serikali ya Mapinduzi Zanziba kwa kushirikiana na Ofisi ya
Makamu wa Kwanza wa Rais tayari imeshaandaa mswaada wa sheria na unasubiri
Baraka za Serikali ili Tume hio iwe na hadhi ya kuwa Mamlaka kamili
Mamlaka ambayo itakuwa na uwezo wa Kisheria wa kuchunguza, kukamata, kupeleleza na kupeleka kesi Mahakamani ambapo sasa Tume inafanya kazi za Kuratibu na Udhibiti wa Dawa za Kulevya kwa kushirikiana na vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama
Aidha
Kanal Burhan amesema Tume imejipanga vyema kulishughulikia na kudhibiti uingizwaji wa dawa za kulevya na ameiomba
jamii kutoa mashirikiano kwa kuwafichuwa wanaojihusisha na dawa za kulevya
ambapo ameahidi Tume kutoa ushirikiano kwa kudhibiti siri za mtoa habari
“Jamii ikithubutu kushirikiana na kubadilisha
mifumo ya maisha ambayo tunaishi ya usasa ni wazi suala la matumizi ya madawa
ya kulevya hapa kwetu litakuwa ni historia, nawaomba wazazi na walezi pia muwe
wadadisi wa watoto wenu na kufatilia mwenendo wao, mtoto anakuja na vespa au
pikipiki mzazi huulizi anarudi usiku huulizi anavitoa wapi vitu vya thamani
hizi ni dalili mbaya na turudi kwenye malezi ya asili”alisisitiza Kanal Burhani
Ziara na ya Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa
Kwanza wa Rais ni muendelezo na utaratibu uliopangwa ili kuona utekelezaji kwa
vitendo wa majukumu ya taasisi zinazosimamiwa na Ofisi hio zikiwemo Baraza la
Taifa la Watu wenye Ulemavu, Tume ya UKIMWI, Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira
na Idara ya Mazingira na Afisi kuu Pemba.
No comments:
Post a Comment