Habari za Punde

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan Aendelea na Ziara yake Siku ya Pili Nchini Misri.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipata maelezo kutoka kwa msimamizi Mkuu wa mradi wa  ujenzi wa mji mpya wa kiserikali wa New Cairo Administrative City unaoendelea kujengwa Jijini Cairo nchini Misri, alipotembeleleo kuangalia maendeleo ya ujenzi wa mji huo leo tarehe 11 Novemba 2021. Mhe Rais Samia yupo Nchini Misri akiendelea na ziara yake ya siku ya pili ya Kiserikali kufuatia mwaliko wa Rais wa Misri Mhe. Abdel Fattah Al Sisi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akitembelea Mji mpya wa New Cairo Administrative City Jijini Cairo nchini Misri  leo tarehe 11 Novemba 2021. Mhe Rais Samia yupo Nchini Misri kwa siku ya pili akiendelea na ziara ya Kiserikali ya siku tatu kufuatia mwaliko wa Rais wa Misri Mhe. Abdel Fattah Al Sisi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiangalia ramani ya mji mpya wa kiserikali wa New Cairo Administrative City unaoendelea kujengwa Jijini Cairo nchini Misri, alipotembeleleo katika Makumbusho mapya yaliopo katika mji mpya wa Kiserikali Cairo Misri leo tarehe 11 Novemba 2021. Mhe Rais Samia yupo Nchini Misri akiendelea na ziara yake ya siku ya pili ya Kiserikali kufuatia mwaliko wa Rais wa Misri Mhe. Abdel Fattah Al Sisi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Baadhi ya Wafanya Biashara nchini Misri alipokutana nao leo tarehe 11 Novemba 2021 Jijini Cairo Misri ambapo amewaelezea fursa mbalimbali ziliopo Tanzania. Mhe Rais Samia yupo Nchini Misri akiendelea na ziara yake ya siku ya pili ya Kiserikali kufuatia mwaliko wa Rais wa Misri Mhe. Abdel Fattah Al Sisi.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akishuhudia utiaji saini Hati za makubaliano  katika Nyanja ya kukuza Uwekezaji kati ya Tanzania na Misri iliyosainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini Dkt. Maduhu Kazi na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya  Uwekezaji na Biashara Huria nchini Misri Dkt. Mohammed Abdul-Wahabi leo tarehe 11 Novemba 2021 Jijini Cairo Misri. Mhe Rais Samia yupo Nchini Misri akiendelea na ziara yake ya siku ya pili ya Kiserikali kufuatia mwaliko wa Rais wa Misri Mhe. Abdel Fattah Al Sisi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa picha ya pamoja na Wafanyabiashara wa Misri baada ya kuzungumza na Wafanyabiashara hao leo tarehe 11 Novemba 2021Jijini Cairo nchini Misri, ambapo amewaelezea fursa mbalimbali za uwekezaji ziliopo nchini Tanzania. Mhe. Rais Samia yupo Nchini Misri akiendelea na ziara yake ya siku ya pili ya Kiserikali kufuatia mwaliko wa Rais wa Misri Mhe. Abdel Fattah Al Sisi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa picha ya pamoja na Wafanyabiashara wa Misri baada ya kuzungumza na Wafanyabiashara hao leo tarehe 11 Novemba 2021Jijini Cairo nchini Misri, ambapo amewaelezea fursa mbalimbali za uwekezaji ziliopo nchini Tanzania. Mhe. Rais Samia yupo Nchini Misri akiendelea na ziara yake ya siku ya pili ya Kiserikali kufuatia mwaliko wa Rais wa Misri Mhe. Abdel Fattah Al Sisi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akishuhudia mabadilishano ya Hati za makubaliano  katika Nyanja ya kukuza Uwekezaji kati ya Tanzania na Misri iliyosainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini Dkt. Maduhu Kazi na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya  Uwekezaji na Biashara Huria nchini Misri Dkt. Mohammed Abdul-Wahabi leo tarehe 11 Novemba 2021 Jijini Cairo Misri. Mhe Rais Samia yupo Nchini Misri akiendelea na ziara yake ya siku ya pili ya Kiserikali kufuatia mwaliko wa Rais wa Misri Mhe. Abdel Fattah Al Sisi.
 PICHA NA IKULU.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.