Habari za Punde

Rais Dk Hussein Mwinyi atuma salamu za rambirambi kwa familia za marehemu wa ajali ya kuzama kwa boti Kisiwa Panza

 

STATE HOUSE ZANZIBAR

OFFICE OF THE PRESS SECRETARY

PRESS RELEASE

Zanzibar                                                                     05.01.2022

---

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ametoa salamu za rambirambi kwa familia za marehemu waliofariki kutokana na ajali ya kuzama kwa boti huko Mkoa wa Kusini Pemba.

 

Katika salamu hizo za rambirambi,  Rais Dk. Mwinyi alieleza kusikitishwa na vifo hivyo na kuzinasihi familia za marehemu hao kuwa na subira na ustahamilivu katika kipindi hiki kigumu cha misiba hiyo.

 

Rais Dk. Mwinyi alimuomba Mwenyezi Mungu awalaze Marehemu wote mahala pema peponi,  Amin.

 

Wakati huo huo, Rais Dk. Mwinyi aliwaombea kwa MwenyeziMungu wale wote waliopata madhara kufuatia tukio hilo kupona kwa haraka.

 

Ajali hiyo imetokea jana jioni (04.01.2022) baada ya boti waliyokuwa wakisafiria wananchi hao kuelekea msibani huko Kisiwa Panza wakitokea Chake Chake Pemba kuzama, ambapo kwa mujibu wa taarifa ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Matar Zahor Masoud, vyombo vya uokozi bado vitaendelea na taratibu za kuwatafuta waliofariki ama wale walionusurika na ajali hiyo.

 

Imetayarishwa na Kitengo cha Habari,

Ikulu Zanzibar

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.