RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alh Dk.Hussein Akli Mwinyi akijumuika na Wananchi katika kisoma na dua kumuombea Marehemu Mchano Mawadi Omar Sheha wa Kwahani, maziko yaliofanyika Kijiji kwao Chaani Masingini Mkoa wa Kaskazini Unguja
Aidha, Rais Dk.
Mwinyi alitumia fursa hiyo kuipa pole familia ya Marehemu Mzee Machano Mwadini
Omar mara baada ya kufika kijijini hapo, na kuinasihi familia kuwa na subira
katika kipindi hichi cha msiba pamoja na kuendelea kumuombea dua marehemu.
Alhaj Dk. Mwinyi
alimuelezea Marehemu jinsi alivyomfahamu na jinsi alivyokuwa nae karibu katika
kazi wakati akiwa Mbunge wa Jimbo la Kwahani tokea marehemu nae akiwa Diwani na
hatimae kuwa Sheha wa Shehia ya Kwahani, nafasi ambayo alikuwa nayo hadi mauti
yanamfika.
Akitoa pole,
Alhaj Dk. Mwinyi alimuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu Mzee Mwadini Omar mahala pema
peponi, Amin.
Mapema, Alhaj Dk. Mwinyi aliungana
na waumini wa dini ya Kiislamu katika sala ya Ijumaa katika msikiti wa
Mwembenjugu (Masjid Iman), ambapo mara baada ya sala hiyo alitoa salamu kwa
waumini na kuwanasihi kuitumia misikiti kwa masuala mbali mbali ya kijamii.
Alhaj Dk. Mwinyi
alisema kuwa misikiti isitumiwe kwa kusali pekee bali itumike pia kwa masuala
ya kijamii ikiwa ni pamoja na kuwasaidia mayatima, wajane, wasiojiweza na kutoa
elimu juu ya matumizi ya dawa za kulevya pamoja na kupambana na udhalilishaji.
Aliwanasihi waumini
kujikinga na mambo mbali mbali katika jamii pamoja na kujikinga katika afya zao
ikiwa ni pamoja na kuwa na mfumo mzuri wa kula kama alivyofundisha Mtume
Muhammad (S.A.W), kufanya mazoezi huku akisisitiza haja ya kujikinga na maradhi
ya UVIKO-19, majanga ambayo mbali ya kuathiri afya pia yameathiri uchumi kwa kiasi
kikubwa.
Sambamba na
hayo, Alhaj Dk. Mwinyi alikubali ombi la uongozi wa msikiti huo la kusaidia ujenzi
wa msikiti wao ambao hivi sasa haukidhi haja kutokana na kuwa mdogo, ombi
ambalo Alhaj Dk. Mwinyi amelipokea na kuahidi kulifanyia kazi.
Imetayarishwa na Kitengo cha Habari,
Ikulu Zanzibar
No comments:
Post a Comment