Habari za Punde

SMZ Kuzifanyika Ukarabati Nyumba za Mji Mkongwe

Na Kijakazi Abdalla  Maelezo Zanzibar.  28/01/2022

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kushirikiana na Wawekezaji wanatarajia kuzifanyia matengenezo nyumba za Mji Mkongwe  ili kuepusha athari  ambazo zitajitokeza baadae.

Hayo ameyasema na Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Mji Mkongwe Zanzibar Bi.Madina Haji Khamis wakati alipofanya ziara na Wajumbe wa Tume ya UNESCO huko Forodhani.

Amesema Serikali imeamua kutengeneza mfuko kutoka Mji Mkongwe na sheria imeshapitisha hivyo utasaidia kuondoa changamoto za majengo hayo.

Amesema  suala la umiliki wa nyumba  hizo ni la Idara ya Nyumba,Wakfu na wamiliki binafsi  ikiwa Mamlaka ya Mji Mkongwe  ni wasimamizi tu.

Akizungumzia Ujumbe wa Tume ya Unesco kufanya ziara katika MjiMkongwe amesema lengo ni kuona changamoto mbalimbali zinazojitokeza na kuwasilisha ripoti mamlaka husika ili  kuzifanyia kazi.

Nae Mshauri wa Sheria Tume ya Taifa Unesco ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  Caroline Joseph amesema tume ya Unesco imeundwa ili kusimamia mikataba iliyoridhiwa na kuitekeleza.

Amesema kuhusu MjiMkongwe amesema Tume ya Unesco imeamuamua kuona mji huo inaingia katika urithi wa dunia.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.