Immaculate Makilika
– MAELEZO, Zanzibar
Shirika la umeme Tanzania TANESCO pamoja na
Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) yameendelea kushirikiana kwa karibu
na kwenye upande wa usafirishaji na biashara ya nishati ya umeme
nchini.
Ikiwa ZECO ni moja ya
wateja wakubwa na muhimu kwa TANESCO ikitajwa kuchangia sehemu kubwa
ya mapato ya TANESCO kiasi cha takribani shilingi billion 91.7 za kitanzania
kwa mwaka.
Akizungumza leo, Februari 13, 2022,
Visiwani Zanzibar, Msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari –
MAELEZO, Gerson Msigwa wakati akitoa taarifa ya wiki kuhusu utekelezaji wa
miradi ya Serikali katika maeneo mbalimbali nchini alisema,
“Mhe. Rais Hussein Ali Mwinyi amekuja na msisitizo wa uchumi wa Buluu ambao
utahitaji matumizi makubwa ya umeme kwa ajili ya viwanda na shughuli nyingine
za uzalishaji, ambapo tayari kumeshaonekana dalili za kuongezeka kwa matumizi
ya umeme Zanzibar.
Hivyo, ili kuendana na juhudi hizo za Mhe. Rais, TANESCO na ZESCO zimeanza mchakato wa haraka wa kuongeza
laini nyingine (marine cable) kutoka Kunduchi mpaka Mtoni Zanzibar
itakayopitisha megawati 200”.
Msigwa alisisitza “TANESCO imeendelea
kuihudumia Zanzibar vizuri kupitia njia za umeme zilizovushwa baharini kuna,
njia ya kutoka Kunduchi kuja hapa Zanzibar ambapo kuna laini mbili za msongo wa
kilovolti 132 (marine cable) ya kwanza ina uwezo wa megawati 50 na ya pili
megawati 100, njia hizi ndizo zinaleta umeme hapa Unguja ambapo mahitaji yake
ni megawati 93.4 mpaka sasa.”
Aliongeza
kuwa kutoka Tanga kuna njia
ya msongo wa kilovoti 33 (marine cable) kwenda Pemba yenye uwezo wa megawati 20 ambapo
matumizi makuu hadi sasa kwa upande wa Pemba ni megawati 13.
No comments:
Post a Comment