Habari za Punde

TANZANIA YAKUBALIANA NA NCHI ZA KUSINI MWA AFRIKA KUUNDA MFUKO WA KUKABILIANA NA WANYAMA WAKALI NA WAHARIBIFU

Mke wa Rais wa Zimbabwe, Dkt. Amai Auxillia Mnangagwa akifungua rasmi Kongamano la Tembo wa Afrika lililofanyika kwenye Hifadhi ya Hwange nchini Zimbabwe. Kulia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akifuatilia hotuba.

Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeingia makubaliano na Nchi za Kusini mwa Afrika kuunda mfuko maalum kwa kila nchi wa kukabiliana na wanyama wakali na waharibifu hususan tembo.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja(Mb) katika Kongamano la Tembo wa Afrika lililofanyika leo katika Hifadhi ya Taifa Hwange nchini Zimbabwe.

“Tumekubaliana kwamba kuwepo na mfuko maalum kwa kila nchi ambao utakuwa mahsusi kwa ajili ya kudhibiti wanyama wakali na waharibifu kama tembo na pia kuwezesha wananchi wanufaike na rasilimali wanyama hao” Mhe. Masanja amefafanua.

Ameongeza kuwa mfuko huo utakapoanzishwa utawanufaisha wananchi wanaoishi pembezoni mwa hifadhi na waathirika wa wanyama hao wanaoumizwa au kuuawa kwa kuwezesha kulipwa fidia .

Mhe. Masanja amesema kuwa sambamba na hilo mkutano huo umelenga kuangalia namna jamii zinazoishi pembezoni mwa maeneo ya hifadhi kuangalia namna zinavyoweza kushirikishwa katika kutunza rasilimali za wanyama hususan tembo.

Aidha, amesema nchi hizo zimekubaliana zisiingiliwe katika maamuzi na nchi za Magharibi kwa kuwa zenyewe ndio zinahusika katika kutunza wanyama hao na pia zinazoathirika na changamoto za wanyama hao.

Kongamano hilo limehudhuriwa na Mawaziri na Maafisa Waandamizi kutoka nchi za Botswana, Namibia, Afrika Kusini, Tanzania, Zambia na Zimbabwe. 

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori (TAWIRI), Dkt. Eblate Mjingo (kulia) na Afisa Wanyamapori Mkuu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Kay Kagaruki wakifuatilia Kongamano la Tembo wa Afrika lililofanyika kwenye Hifadhi ya Hwange nchini Zimbabwe.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) (kulia) na Mawaziri kutoka Zambia na Botswana wakiagana na Mke wa Rais wa Zimbabwe, Dkt. Amai Auxillia Mnangagwa (kushoto) baada ya kufungua rasmi Kongamano la Tembo wa Afrika lililofanyika kwenye Hifadhi ya Hwange nchini Zimbabwe.


Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeingia makubaliano na Nchi za Kusini mwa Afrika kuunda mfuko maalum kwa kila nchi wa kukabiliana na wanyama wakali na waharibifu hususan tembo.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja(Mb) katika Kongamano la Tembo wa Afrika lililofanyika leo katika Hifadhi ya Taifa Hwange nchini Zimbabwe.

“Tumekubaliana kwamba kuwepo na mfuko maalum kwa kila nchi ambao utakuwa mahsusi kwa ajili ya kudhibiti wanyama wakali na waharibifu kama tembo na pia kuwezesha wananchi wanufaike na rasilimali wanyama hao” Mhe. Masanja amefafanua.

Ameongeza kuwa mfuko huo utakapoanzishwa utawanufaisha wananchi wanaoishi pembezoni mwa hifadhi na waathirika wa wanyama hao wanaoumizwa au kuuawa kwa kuwezesha kulipwa fidia .

Mhe. Masanja amesema kuwa sambamba na hilo mkutano huo umelenga kuangalia namna jamii zinazoishi pembezoni mwa maeneo ya hifadhi kuangalia namna zinavyoweza kushirikishwa katika kutunza rasilimali za wanyama hususan tembo.

Aidha, amesema nchi hizo zimekubaliana zisiingiliwe katika maamuzi na nchi za Magharibi kwa kuwa zenyewe ndio zinahusika katika kutunza wanyama hao na pia zinazoathirika na changamoto za wanyama hao.

Kongamano hilo limehudhuriwa na Mawaziri na Maafisa Waandamizi kutoka nchi za Botswana, Namibia, Afrika Kusini, Tanzania, Zambia na Zimbabwe.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.