Habari za Punde

Waumini wa Dini ya Kiislam Watakiwa Kumuomba Mwenyezi Mungu Ili Aifanye Dunia Kuwa na Amani na Kuondoka Changamoto za Kiuchumi.

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Mahmoud Mussa Wadi (kushoto kwa Rais) alipowasili katika viwanja vya Masjid Ashuraa Umbuji Wilaya ya Kati Unguja kuhudhuria Sala ya Ijumaa na (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe.Hadid Rashid Hadid.

WANANCHI wa Kijiji cha Umbiji Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusin Unguja wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi.(hayupo pichani) akizungumza na kuwasalimia baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa iliyofayika katika Masjid Ashuraa Umbuji leo 27-5-2022.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiitikia dua ikisomwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Saleh Omar Kabi (kulia kwa Rais) baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masjid Ashuraa Umbuji Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja leo 27-5-2022

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na kuagana na Wananchi wa Umbuji baada ya kumalizika kwa Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masjid Ashuraa Umbuji Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja leo 27-5-2022

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi amewataka waumini wa Dini ya Kiislamu kuendelea kumuomba Mwenyezi Mungu ili aifanye dunia kuwa na amani na kuondokana na changamoto za kiuchumi.

Alhaj Dk. Mwinyi ametoa wito huo katika nasaha alizozitoa kwa waumini walioshirki ibada ya Sala ya Ijumaa, iliofanyika Masjid Shura Umbuji, Mkoa Kusini Unguja.

Amesema vita vinavyoendelea kati ya Russia na  Ukrane, ugonjwa wa Covid-19, pamoja na upandaji wa bei ya Mafuta vimesababisha baadhi ya bidhaa muhimu kupanda bei na kupelekea athari kubwa za kiuchumi Dunia.

Aidha, aliwataka wananachi kuendeleza umoja na mshikamano kwa kigezo kuwa mambo hayo huleta amani  na kuwa chachu ya maendeleo.

Alieleza kuwa katika hali ilivyo hivi sasa, jamii haizingatii umuhimu wa  mambo hayo  kwa vile nchi iko katika hali ya amani.

Sambamba na hayo, Alhaj Mwinyi alisisitiza umuhimu wa wananchi kufanya kazi kwa bidii katika kujitafutia maendeleo.

Katika hatua nyengine, Alhaj Dk. Mwinyi amepokea maombi ya wananchi wa Umbuji ya kusaidia upatikanaji wa Zulia, Kipaza sauti pamoja na matengenezo ya Mnara wa Maji wa Masjid Shura.

Nae, Katibu Mtendaji Ofisi ya Mufti wa Zanzibar Sheikh Khalid Ali Mfaume aliwataka waumini hao kuendelea kumuombea Dua Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Mwinyi, ili aweze kutekeleza vyema majukumu yake ya kuwaletea maendeleo wananchi.

Mapema, Khatibu katika Sala hiyo ya Ijumaa Sheikh Idd Mrisho Vuai aliwataka waumini kuzingatia umuhimu wa kushikamana, kupendana na kushirikiana,  ak  kuepuka chuki, bughudha na ugomvi, sambamba na  kusistiza haja kushikamana na mafunzo ya Mtume Muhamad (SAW).

Wakati huo huo, Rais Alhaj Dk. Mwinyi alipata fursa ya kufika nyumbani kwa Mbunge wa Jimbo la Amani Mussa Hassan kwa jili ya kutoa mkono wa pole kutokana na kifo cha Baba yake mzazi. 

Imetayarishwa na Idaya ya Mawasiliano

Ikulu Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.