Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Hussein Ali Mwinyi alisema
hayo wakati wa halfa ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya miaka 25 ya Mfuko
wa Fursa Sawa kwa Wote (EOTF), Jijini Dar es Salaam.
Dk
Mwinyi alisema hayo yanafanyika kwa kuwa jukumu la serikali zote ni kuandaa
mazingira yatakayowezesha sekta binafsi na asasi za kiraia kushiriki katika
kufanikisha utekelezaji wa mipango ya maendeleo.
Alisema
program za kuwezesha wanawake wajasiriamali, elimu na afya za EOTF ni muhimu
kwa maendeleo ya nchi.
“Ile
ya kupambana na umaskini kwa makundi mbalimbali ya wanawake ina umuhimu wa
pekee, ikizingatiwa kwamba kuna changamoto nyingi za kiuchumi na kijamii
zinazoyakumba makundi mbalimbli ya wanawake ambao ndio idadi kubwa ya nguvu
kazi kwa taifa letu,” alisema.
Kwa
mujibu wa Rais Mwinyi, juhudi za kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa kuwapatia
mitaji, elimu na kuwatafutia masoko ya bidhaa zao ni muhimu katika kuondoa
changamoto ya ajira inayoathiri kundi kubwa la wanawake na vijana hivi sasa.
“Ni
ukweli usio na shaka kwamba serikali zetu haziwezi kuajiri vijana wote
wanaomaliza masomo yao katika ngazi mbalimbali. Ni lazima tuwape njia na mbinu
mbadala za kujiajiri kama inavyofanywa na mfuko huu.
“Vile
vile program nyingine mbili mnazoziendesha katika sekta ya afya na elimu nazo
zina umuhimu mkubwa, tukizingatia kwamba, ili tuweze kujenga taifa bora, ni
lazima tuwe na nguvu kazi yenye afya na elimu inayoendana na wakati na mahitaji
tuliyonayo,” alisema
Dk
Mwinyi alisema EOTF ni mdau muhimu wa serikali katika kuimarisha ustawi
wa watoto, vijana na wazee wa jinsia zote.
“Kama
tujuavyo serikali ina majukumu mengi na mzigo mkubwa wa kutekeleza mipango yake
ya maendeleo na utoaji wa huduma kwa wananchi.
“Kwa
hiyo misaada inayotolewa na asasi zisizo za kiserikali za kitaifa, kikanda na
kimataifa pamoja ile inayotolewa na washirika wa maendeleo ni muhimu ili kuweza
kufikia malengo yetu,” alisema.
Alisema
mfuko huo ni mfano bora wa ushirikiano na serikali unaopaswa kuigwa na asasi
nyingine za kiraia za ndani nan je ya nchi.
Awali
Mwenyekiti wa mfuko huo Anna Mkapa alisema kwa miaka 25 wamekuwa mstari wa
mbele katika nyanja ya kuondoa umaskini kwa wanawake kwa kuwawezesha
wajasiriamali 6,000 kutoka Bara na Visiwani kupata mafunzo ya ujasiriamali,
Pia
kutangaza na kuuza bidhaa zao kupitia maonyesho mbalimbali na kujipatia zaidi y
ash trilioni 11, ikiwa ni pamoja na kuzalisha ajira zaidi ya 25,000.
program
nyingine aliyoitaja ni kusaidia kwenye elimu kwani imetoa ufadhili kwa watoto
1755 kutoka kwenye familia duni kupata elimu kutoka chekechea, shule za msingi,
sekondari, Veta hadi vyuo vikuu vya ndani na nje.
Alieleza
Program nyingine ni ya afya ambayo imesaidia mama na mtoto kwa kujenga
hospitali, zahanati, vituo vya afya, magari ya kubebea wagonjwa, vifaa vya
hospitali, viti mwendo kwa hospitali, shuleni na watu binafsi.
Alisema
pia katika kutatua tatizo la watoto yatima na wa mitaani katika jamii,
wamejenga kituo cha watoto yatima Mtaa wa Simbani Kibaha.
No comments:
Post a Comment