Habari za Punde

Sensa Haihusiani na Siasa Bali ni Mhimili wa Maendeleo ya Taifa.

Na Mwashungi Tahir- Maelezo 02/08/2022

Vyama vya siasa Zanzibar vimetangaza rasmin kushiriki katika Sensa ya Watu na Makaazi ifikapo tarehe 23 Ogasti 2022.

 

Wakizungumza katika Mkutano maalum uliofanyika katika ukumbi wa Takwimu Mazizini wamesema ili serikali iweze kupanga mipango yake kwa usahihi ya kuwaletea Wananchi maendeleo ,ni vyema kuungana  pamoja katika  kuhesabiwa ili ipatikane idadi kamili

 

Wamesema sensa haihusiani na siasa Bali ni  mhimili wa maendeleo ya Taifa hivyo ni vyema kwa  wanachama nao wakaashiriki kutoa taarifa sahihi wakati karani wa sensa atakapofika katika nyumba zao .

 

Aidha wamesema  itikadi zao za kisiasa  kwa sasa zimeweka kipaumbele  maslahi  ya taifa kwa lengo la kuipa nguvu serikali katika kupanga mipango yake ya kiuchumi ya miaka kumi ijayo Kama yalivyo malengo endelevu ya mkakati wa Dunia.

 

Sensa ya mwanzo ilifanyika nchini katika mwaka 1967 ikiwa moja ya mataka ya kimataifa kuhakikisha  Serikali inaandaa, kupima na kutathmini utekelezaji wa maendeleo yake

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.