Habari za Punde

Ufunguzi wa Kongamano la Uwekezaji la Kiuchumi Zanzibar

 

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman , akizungumza katika Ufunguzi wa Kongamano la Bishara kati ya Zanzibar  na Italy  huko hoteli ya Golden Tulip leo tarehe 28.09.2022. Mhe. Makamu alimuawakilisha rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Mwinyi.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman , akizungumza katika Ufunguzi wa Kongamano la Bishara kati ya Zanzibar  na Italy  huko hoteli ya Golden Tulip leo tarehe 28.09.2022. Mhe. Makamu alimuawakilisha rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Mwinyi
Baadhi ya washiriki wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji  kati ya Italy na Zanzibar  wakimsikilia Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akisoma hotuba ya Ufunguzi wa Kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tilip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi "B" Unguja ,Mhe. Othman alimuwakilisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali  Mwinyi. 
Baadhi ya washiriki wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji  kati ya Italy na Zanzibar  wakimsikilia Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akisoma hotuba ya Ufunguzi wa Kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tilip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi "B" Unguja ,Mhe. Othman alimuwakilisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali  Mwinyi. 
 ( Picha na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar).

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othaman, amesema kwamba            Zanzibar imefungua vyema milango zaidi ya uwekezaji kwa nia ya kufanikisha na kukuza uchumi na maendeleo ya Zanzibar.                                                                           

Mhe. Makamu ameyasema hayo huko hoteli ya Park Hyatt Shangani mjini Zanzibar, katika hotuba yake ya ufunguzi wa Kongamano la Uwekezaji  kati ya Marekani na Tanzania.

Amesema kutokana na dhamira hiyo,  hivi sasa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imerahisisha  taratibu za maombi  ya uwekezaji na kwamba  kibali kinaweza kupatikana ndani ya kipindi kifupi cha kumuwezesha muwekezaji ama mfanyabiashara kuendelea na shughuli zake za kibishara kwa wepesi.

Mhe. Othman amefahamisha kwamba kongamano hilo linalojumisha wataalamu,  kutoka nchi tofauti ikiwemo Kenye, Afrika Kusini , Tanzania na Marekani ni muhimu kwani wataweza kujadili changamoto zilizpo na kupendekeza njia bora za kuzitatua ili kuleta maendeleo ya biashara na uwekezaji Zanzibar.

Aidha Mhe. Othman amepongeza juhudi za rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mama Samia Suluhu Hasan na Rais wa Zanzibar Mhe. Dk Hussein kwa Juhudi zao za kuitaingaza nchi kiutalii kupitia filamu ya Royal Tours iliyozinduliwa Marekani Mwezi Aprili mwaka huu wa 2022.

Amesema hatua hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa ndani ya kipindi kifupi kujitokeza wawekezaji  wengi na kuongezeka uwekezaji wa kibiashara ndani ya Tanzania Bara na Zanzibar ikiwa ni matokeo ya filamu hiyo.

Mhe. Othman ameongeza kwamba  juhudi hizo zimechangia  kuwezesha Tanzania hivi sasa kwa na  jumla ya Kampuni  kubwa 19 za kibiashara kutoka Marekani  na wameweza kuwekeza kwa mtaji wa  kiasi cha dola trilioni 1.6.

Aidha amesema kwamba pia sera ya uchumi wa Buluu  iliyoasisiwa  hapa Zanzibar inalenga  kuzitumia vyema fursa na rasilimali za baharini  huku ikiweka mazingatio makubwa katika suala la uhifadhi na usimamizi wa mazingira yasichafuliwe.

Pia Mhe. Othman amesema kwamba Serikali imefanya marekebisho ya sheria yake namba 14 ya mwaka 2018 ya Mamlaka ya Kuendeleza na Kukuza Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA) na kulitenga eneo la Pemba kuwa ni maalumu kimkakati katika uwekezaji.

Amefahamisha kwamba kutokana na hali hiyo sheria hiyo imeweka vivutio maalum kwa wewekezaji wote watakaokwenda kuwekeza katika eneo la Kimkakati la Micheweni Pemba na kwamba jambo hilo linania la kusaidia eneo hilo kuendelezwa zaidi kibiashara.

Naye waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar , Omar Said Shaaban amesema kwamba serikali inafanya juhudi ili kuiwezesha sekta ya  maendeleo ya bishara kwenda sambamba na mahitaji ya wataalamu wanaohitajika katika sekta hiyo.

Amesema ujio wa Kampuni zaidi ya 20 kutroka Marekani zilizoshiriki katika Kongamano hilo ni hatua kubwa katika kukuza sekta ya biashara na kuongeza fursa za upatikanaji wa ajira nchini.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi, Ajira na Uwekezaji, Zanzibar Mhe. Mudrik Ramadhan Soraga, amesema kwamba mkutano huo ni muhimu katika kuainisha fursa na changanoto zilizopo katika jitihada za kukuza sekta hiyo nchini.

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo cha Habari leo tarehe 28.09.2022.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.