RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,
Dk. Hussein Ali Mwinyi alisema tatizo la mfumko wa bei za bidhaa na huduma kwa
wananchi ni suala mtambuka ambalo huchangiwa na sababu nyingi zikiwemo mfumko
wa bei ulimwenguni kutokana na mabadikilo ya dunia ikiwemo vita vya Urusi na
Ukrain sambamba na changamoto zinazobasabishwa na ufinyu wa bandari ya
Zanzibar.
Alisema kupanda
kwa bei za bidhaa sio tatizo liliopo Zanzibar pekee lakini ametolea ufafanuzi
kwa sababu zilizo ndani ya mamlaka za serikali kuchukuliwa hatua za haraka ili
kupunguza ukali wa maisha ikiwemo kuboresha ufanisi na utendaji wa utoaji
huduma kwenye bandari ya Zanzibar ili kupunguza athari kali kwa wananchi.
Dk. Mwinyi
aliyasema hayo wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari kwenye mkutano wake
na waandishi hao anaoufanya kila mwisho wa mwezi kwa kuzungumza nao pamoja na
wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini.
“Kuhusu
kupanda kwa bei za bidhaa, nataka niseme kwamba ziko sababu nje ya uwezo wa Serikali
hatuna jinsi, zikiwemo kupanda kwa bei za bidhaaa huko zinakotoka, kuna baadhi
ya mataifa wamezuia kuuza bidhaa zao nje ya nchi kwaaajili ya kujiwekea akiba
kutoka na vita wa Urusi na Ukrain hali iliyochangia kupungua kwa uingizwaji wa
bidhaa nchini, hayo na mengine ndio yanayosababisha bidhaa za chakula duniani
kupanda sio Zanzibar peke yake” alifafanua Dk. Mwinyi.
Akizungumzia
mfumko wa bei kwa bidhaa za Zanzibar, Dk. Mwinyi alieleza bidhaa nyingi za
vyakula zinatoka Tanznaia bara ambako pia bidhaa zimepanda bei kutokana na
ukame ulioikumba baadhi ya mikoa nakuongeza kuwa ukame umepunguza uingizwaji wa
bidhaa na kusababisha bidhaa chache ziliopo kupanda bei sambamba nakueleza changamoto
zinazisababishwa na bandari ya Zanzibar ikiwemo ufinyu wa mazingira ya bandari ya
malindi hali aliyoielezea kuchangia kuzorotesha zoezi la kushushwa kwa mizigo
bandarini hapo.
“Bandari
yetu ufanisi wake ni mdogo sana, sababu ina gati moja, meli zinakuja zinakaa
sana, zikifuatana meli tatu nne, wa mwisho atashusha mzigo baada ya mwezi
mmoja” alibainisha Rais Mwinyi.
Alisema,
Serikali imechukua hatua ya kupunguza baadhi ya changamoto ikiwemo kutumia
bandari ya Mangapwani ili kupunguza msongamano kwenye bandari ya Malindi na
kutoa wepesi wa bidhaa nyingi kushushwa kwa wakati na kuwafikia wahitaji ambao
ni wananchi.
Akizungumzia
suala la maadhimisho ya sherehe za miaka 59 ya Mapinduzi ya Zanzibar Dk. Mwinyi
alisema kwa mwaka 2023 hakutakua na sherehe kubwa badala yake gharama
zilizopangwa kuadhimisha sherehe hizo zitaelekezwa kwenye miradi ya maendeleo
ambapo Dk. Mwinyi alieleza fedha hizo zimepelekewa kuongeza nguvu Wizara ya Elimu.
Alieleza,
awali sherehe za Mapinduzi zilipangwa kutumia milioni 700 licha ya gharama
kupunguzwa hadi kufikia 450 milioni ambazo fedha hizo Rais Mwinyi alesema
Serikali imezielekeza kuongeza nguvu kwenye miradi ya sekta ya Elimu ikiwemo
kuongezwa kwa maradasa, madawati, maabara na huduma nyengine za elimu.
Kuhusu
sekta ya Afya, Dk. Mwinyi alieleza katika kuboreshwa huduma za Afya kwenye
vituo vya afya, Serikali imekuja na utaratibu mpya wa kutoa huduma kwa
kushirikiana na sekta binafsi ili kuboresha huduma bora kwa wananchi nakuongeza
kuwa Serikali kupitia hospitali za Wilaya na Mikoa zitatoa huduma zote na suala
la huduma za maabara zimeelekezwa kwenye sekta binafsi ili kuipa wepesi serikali
kuwahudunia zaidi wananchi.
“Sekta
ya afya tumekuja na utaratibu mpya wa kutoa huduma zifanywe na sekta binafsi
(outservices), kwa hivyo maabara za hospitali hizi mpya za wilaya na mikoa
huduma zitatolewa na sekta binafsi, lile suala la mashine imeharibika sasa hivi
hakuna tena, huduma zote za vipimo vya X -ray, MRI na huduma nyengine za
kimaabara zimepelekwa huko” Alifafanua Dk.Mwinyi.
Kuhusu
kutatua changamoto ya ajira nchini, Dk. Mwinyi alieleza tayari serikali
imezungumza na balozi zake zilizo nje ya nchi ilikuangalia uwezekano wa
kuwapata mawakala wa ajira na kuweka taratibu rasmi za ajira ili kukwepa lawama
za baadae na ukiukwaji wa haki za binaadamu zinazovunjwa na baadhi ya waajiri
kwa baadhi ya nchi.
“Tumeshazungumza
na mabalozi wetu, watutafutie wale watu wanaoajiri tuwaunganishe na mawakala wa huku ili vijana
wetu waweze kufanyakazi nje” alifafanua Rais Mwinyi.
Rais Dk.
Mwinyi, amekua akitumia utaratibu wa kuzungumza na waandishi na wahariri kutoka
vyombo mbalimbali vya habari nchini ikiwa ni utaratibu wake wa kusikiliza na
kutatua moja kwa moja changamoto zinazowakabili wananchi ambao baadhi yao
humfikishia Mhe. Rais kupitia vyombo hivyo, na huu ni mkutano wa mwisho kwa
mwaka 2023.
Imetayarishwa na Idara ya Mawasiliano
Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment