Habari za Punde

Ofisi ya Waziri Mkuu Yapokea Maoni Kuhusu Rasimu ya Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya Mwaka 2022

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Prof. Jamal Katundu akitoa maelezo ya awali kwa wadau juu ya umuhimu na faida za kupitia Rasimu ya Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya Mwaka 2022 wakati wa kikao kazi kilichofanyika jengo la OSHA, leo Disemba 06, 2022, jijini Dodoma.

Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu imepokea maoni kuhusu Rasimu ya Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii kutoka kwa wadau wa sekta ya hifadhi ya jamii wakati wa kikao kazi kilichofanyika jengo la OSHA, leo tarehe 06 Disemba, 2022, jijini Dodoma.

Aidha, hatua ya maandalizi ya Sera hiyo mpya ni kufuatia Sera ya awali ya hifadhi ya jamii ya mwaka 2003 kutofanyiwa mapitio/maboresho kwa muda mrefu, hali iliyopelekea uhitaji wa sera hiyo mpya ambayo itaendana na mabadiliko mbalimbali katika sekta ya hifadhi ya jamii.

 

Wadau wa Sekta hiyo wameweza kutoa maoni juu ya rasimu ya Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2022 katika Kikao kazi hicho kilichoongozwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Prof. Jamal Katundu.  

 

Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu kupitia Idara ya Hifadhi ya Jamii na Idara ya Sera na Mipango zinaratibu maandalizi ya Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2022.

 

Wadau walioshiriki kikao kazi hicho ni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma akichangia jambo wakati wa kikao kazi hicho.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Bw. Bernard Konga akieleza jambo wakati wa kikao kazi hicho cha kutoa maoni kuhusu Rasimu ya Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya Mwaka 2022, kilichofanyika Jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Said Mabiye (kulia aliyesimama) akiwasilisha Rasimu ya Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya Mwaka 2022 wakati wa kikao kazi hicho kilichofanyika jengo la OSHA, leo Disemba 06, 2022, jijini Dodoma.
Baadhi ya wadau walioshiriki kikao kazi cha kupitia rasimu ya Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Prof. Jamal Katundu (hayupo pichani).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.