Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Sheria Ndogo imepokea taarifa ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kuhusu
hoja mbalimbali za uchambuzi kuhusu Kanuni ziitwazo Licensing and Rights To
Benefit From Re- Sale, Regulations ambazo zimeanzishwa na Sheria ya
HakiMiliki na Hakishiriki.
Akiwasilisha Taarifa hiyo,
Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Pauline Gekul amesema, wizara
imefanyia kazi hoja mbalimbali ilizoagiza
na Bunge katika vikao vya Kamati vya mwezi Aprili 2022.
"Wizara imepokea Hoja
06, kutoka katika Kamati na imezifanyia kazi
kupitia Ofisi ya Hakimili na Hakishiriki ( COSOTA) ikiwemo kuzifuta
baadhi ya Kanuni na kutengeneza nyingine
ambazo zipo Ofisi ya mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kuhakikiwa na
kupewa kibali" amesema Mhe.Gekul.
Kwa upande wake Mwenyekiti
wa Kamati hiyo Mhe.Gaston Rwekiza ambaye ni Mbunge wa Bukoba Vijini ameelekeza
wizara kukamilisha mchakato wa kutengeneza Kanuni hizo, mapema na kuziwalisha
kwa Kamati hiyo kwa ajili ya hatua zinazofuata.
Kikao hicho kimehudhuriwa na
Naibu Katibu Mkuu Said Yakubu, Afisa
Mtendaji Mkuu wa COSOTA Bi. Doreen
Sinare na Viongozi wengine wa Wizara.
No comments:
Post a Comment