MAKAMU wa Kwanza
wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amezitaka Taasisi za Mafunzo ya
Amali, Watoa huduma, pamoja na Wajasirimali nchini kujitahidi kuzitangaza
shughuli wanazofanya ili ziweze kufahamika vyema na jamii na watumiaji wengine
mbali mbali wa ndani na nje ya nchi.
Mhe. Othman
ametoa wito huo huko katika Viwanja Maisara mjini Zanzibar, alipotembelea
mabanda mbali mbali ya maonesho ya Biashara ikiwa ni shamra shamra za sherehe
za Mapituzi ya Zanzibar ya Januari 1964 kutimiza miaka 59.
Mhe. Makamu
amefahamisha kwamba zipo shughuli nyingi nzuri na zenye manufaa makubwa
zinazofanywa na wajasiramali, utaalamu kutoka Taasisi za Elimu na pamoja na
shughuli za watoa huduma lakini hazifahamiki ipasavyo kutokana na kutotangazwa
vyema.
Amefahamisha
kwamba kuwepo kwa maonesho hayo ni fursa muhimu za kutangaza na kuonmesha hatua
kubwa za utaalamu na uzalishaji wa bidhaa zilizofikiwa kutoka taasisi mbali
mbali nchini na kwamba kutangazwa ipasavyo kutasaidia vyema kueleweka na wenye
mahitaji kuweza kuzitumia.
Aidha
amezikumbusha taasisi za Elimu na hasa Vyuo vya Amali na na wazalishaji bidhaa
za biashara kuzalisha bidhaa zenye kukubalika katika masoko ya ndani nanje sambamba na kuzalisha wataalaum wanaokubalika
na kukidhi matakwa ya soko hasa katika sekta ya Utalii inayoendelea kukua kwa
kasi kubwa na mahitaji ya wataalamu kwa fani mbali mbali kuongezeka.
Akitembelea
Banda la Utafiti wa Mifugo Mhe. Othman, ameshari Taasisi hiyo kujenga uwezo wa
ndani kiutalam, ili kuweza kuzalisha
chakula cha mifugo ya aina mbali mbali inayohitajika hapa nchini.
Naye
Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti wa Mifugo Zanzibar Nd. Talib Ali Suleima,
amesema kwamba malighafi nyingi zinazotumika kutayarisha na kuzalisha chakula
cha mifugo ya aina mbali mbali zinatoka nje ya Zanzibar jambo ambalo linaongeza
gharama kwa bidhaa hizo.
Naye Ofisa
Mwandamizi wa kutoka Idara ya Utafiti wa Mifugo nchini Zuhera Karim Zam , amesema
kwamba asilimia kubwa ya chakula cha mifugo kinatokana na bidhaa za kilo, huku
wakulima wengi wa Zanzibar wakizalisha bidhaa chache na kulazimika kununa nje
ya nchi jambo lonaloongeza gharama za bidhaa hizo.
Kwa upande
wake Mkurugenzi Mtedaji wa Mamlaka ya Vyuo vya Amali Zanzibar Dk. Bakari Ali
Silima, amesema kwamba Mamlaka hiyo inawasiliana na watumaiaji wataalamu wa
sekta ya Utalii ambao ni wamiliki wa mahoteli mbali mbali ili kueleza aina na
haja ya wataalamu wanaowahitaji katika tasinia ya Hoteli nchini.
Amefahamisha
kwamba kwa mujibu wa wamiliki hao, hoteli nyingi zinahitaji wataalamu wenye
ujuzi mchanganyiko katika fani za utaalamu zaidi ya mbili ili waweze kuajirika
na kutumika vyema kwenye ajira wanazopewa, jambo ambalo limezingatiwa ipasavyo
na Mamlaka hiyo katika fani wanazofundisha nchini.
Kwa upande
wake Mkurugenzi wa MoroBatik Dk. Marieta Mkanga, ameiomba serikali kupunguza
ama kuonsha kabisa kodi za bidhaa za batiki wanazotumia kuzalisha mashati,
mikoba na magauni na bidhaa nyenginezo ili
uzalishaji wao uweze kuwa na gharama nafuu na kuweza kuhimili ushindani
wa soko la ndani na nje kwa bidhaa za aina hiyo.
Imetolewa
na Ofisi ya Makumu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha
Habari Tarehe 11.01.2023
No comments:
Post a Comment